Рет қаралды 96
Niliwahi kusema na hapa nataka nirudie tena kwa msisitizo, ukimya wangu siyo ujinga, na wala kuzungumza sana siyo werevu hata kidogo. Kuzungumza sana ni udebe tupu tu haliachi kuvuma na lazima litavuma, na anayenyamaza kimya siyo mjinga. Ni mtu anayetafakari mambo, si ujinga. Kwa hiyo ukimya wangu si ujinga na kuropokwa kwao si werevu. Mliponikabidhi dhamana hii niliapa kulinda na kuitetea katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, na dhamana yangu pamoja na vyombo vya ulinzi ni kulinda amani ya nchi yetu. Hivyo sitokuwa na muhali kwa yeyote anayetaka kuvuruga amani hiyo ya nchi yetu. Tumevumiliana kwenye mengi lakini kwenye kulinda tunu ya amani na utulivu wa nchi, nirudie tena sitakuwa na muhali kwa yeyote atakayejikaribisha katika mambo haya. Anayeratibu, anayeshiriki hata anayetekeleza mipango hiyo miovu,” Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
--
Dar24 ni chanzo namba moja cha habari kwa watanzania mahali popote walipo duniani. Kwa habari za uhakika kutoka nyanja mbali mbali.
JE, NA WEWE UNA HABARI?
⚫️ WASILIANA NA DAR24 MEDIA: +255 679 979 786
⚫️ Email: dar24newsroom@gmail.com
⚫️ Website: www.dar24.com
⚫️ Instagram: @Dar24news
⚫️ Facebook: @dar24
⚫️ Twitter: @Dar24News