Рет қаралды 10,155
Wenyeji wa kijiji cha Msomera wanadai wameporwa ardhi yao na kupewa wahamiaji kutoka Ngorongoro, Serikali imejibu tuhuma hiyo.
Jamii ya wafugaji wa kabila la kimaasai, ambao ni wenyeji wa kijiji cha Msomera, wilayani Handeni, mkoani Tanga nchini Tanzania, wanadai haki yao ya umiliki wa ardhi, baada ya serikali kuchukua ardhi yao na kuipangia matumizi mbalimbali ya miradi ya maendeleo na makazi kwa watu takribani 3,010 waliohamishwa kutoka hifadhi ya bonde la Ngorongoro.
Wenyeji hao wa Msomera, wanaitaka serikali kuacha mara moja kile wanachokiita uporaji wa ardhi yao wanayoimiliki kihalali, na wanaitaka serikali kusitisha mpango wa uhamishaji wa wafugaji kutoka Ngorongoro kutokana na ukwei kwamba, wageni hao wanaweza kusababisha hasira, chuki, uhasama na mgogoro mbaya wa kugombea ardhi ya malisho na makazi.
URAIA TV imefanya uchunguzi wa kina wa mgogoro huo, na kuandaa makala hii.