Рет қаралды 327
Kwasasa Taifa linapitia katika changamoto ya mafuta ya kupikia ambapo gharama zake zimekuwa kubwa sana kulinganisha na kipindi cha nyuma zao hili wenda likawa ufumbuzi wa changamoto ya mafuta endapo serikali ikiweka mkono wake kwa asilimia kubwa.
Bw.Jesse Oljange ambaye ni Mkurugenzi mwendeshaji wa Avomeru Group alisema kwamba waliweza kufanya utafiti wa matunda ya parachichi na kugundua matunda hayo yana vitu vingi wanavyoweza kuvitumia kuzalisha bidhaa nyingine
"Baada ya kufanya maboresho katika miche kwa sasa mti mmoja unatoa kg 40 hadi 50 kwa mwaka wa kwanza na hadi kufikia mwaka wa tatu mti huo unauwezo wa kutoa kg 300 na kuendelea na imekuwa na mafanikio makubwa sana kwa wakulima". Alieleza Jesse