Рет қаралды 21,893
Hali ya taharuki imetanda katika eneo la Kigumo kaunti ya Muranga baada ya wakazi kuvamia kituo cha polisi cha Gachocho na kumuua mshukiwa wa mauaji aliyekuwa akizuiliwa na polisi. Wakazi wa eneo hilo waliojawa na ghadhabu waliwashinda nguvu polisi waliojaribu kuwatawanya kwa kutumia vitoa machozi kabla ya kuingia ndani na kumuua richard maina anayedaiwa kuhusika na mauaji ya nduguye