Рет қаралды 20,967
Watu wanane wanauguza majeraha baada ya kuvamiwa na genge la wahuni usiku wa kuamkia leo katika eneo la Mikindani eneo bunge la Jomvu kaunti ya Mombasa. Genge hilo linadaiwa kujihami kwa mapanga lilitekeleza uvamizi huo mwendo wa saa saba usiku kabla ya kutoweka. Maafisa wa polisi wanaendeleza msako ambapo inaarifiwa washukiwa wanne wa genge hilo wamekamatwa.