Nani anasikiliza hiki chuma August 12, 2024... Dizasta mtu mbaya sana
@dizastavina3 жыл бұрын
“JASIRI JOHN….. ALIYAANGALIA MAISHA YAKE HAKUONA JINSI ANGEWEZA KUISHI BILA JANE MSICHANA ANAYEMPENDA LICHA YA KUZONGWA NA UMASIKINI ALIJITAHIDI KUMPA JANE MAHITAJI MADOGOMADOGO KADRI ALIVYOWEZA LAKINI ALIFAHAMU SHUBIRI YA KUSUBIRI KUPENDWA HUKU ANAFAHAMU KUSUBIRI KUPENDWA NI MATUMAINI YANAYOUMIZA. KAMA WANAVYOSEMA, MTAFUTAJI HACHOKI AKICHOKA KASHAPATA… .ALIENDELEA KUNGOJA” Ah! Sikuwa na zali sikuziamini ndumba Sikuwa na mali za kufuja Nilijitahidi kuuza mitumba kufuga mipunga Ili siku nimpe gari nimpe nyumba. Nilishindwa… Niliishia kumpa chai, ‘chipsi’ mayai na ‘vocha’ Nywele za kimasai na mkoba Pesa za magauni, majuba na viatu vya kuzuga Nilimpa muda ila bado haikutosha, kwani… Nilipomwambia nampenda hakujibu Akaweka moyo wangu maumivu Na mtima wangu akauweka ‘solemba’ Nikaapia kuwa sitakuja kupenda ‘forever’ Ah! Nilimpa upendo nilimpa sifa Niliweka mitego ya faida, haikuwa shwari Nikabadili mwenendo wa maisha Niliweka malengo sikutimiza, hakunikubali Alikuwa na ndoto kubwa kushinda mimi Alikuwa na misimamo kuipita dini Aliniambia ameomba nije kuokota utajiri Amengoja sana na sasa amechoka kusubiri “JOHN ALIFAHAMU HALI YA JANE, KUWA JANE ALIZALIWA KWENYE FAMILIA MASIKINI, NA ALIUCHUKIA MNO UMASIKINI. ALIFAHAMU UMASIKINI ULIVYOCHUKUA UHAI WA MAMA YAKE KIPENZI, ALIYEFARIKI KWA KUKOSA MATIBABU. ALIIFAHAMAU NADHIRI ALIYOIWEKA JANE YA KWAMBA HATOKUBALI TENA KUISHI KWENYE MAISHA YA KIMASIKINI, NADHIRI ILIYO MWEKA JOHN NJIAPANDA” Ah! Sikuwa na hali ya kuikosha roho yake Nilimwacha aende aufate moyo wake Alipata bwana wa kizungu magharibi Alimwahidi kuishi maisha ya ndoto zake Nilipata uchungu niliishia kuhamaki nilitaka nijiue Nilitaka nimzuie abaki nikakumbuka Ukipenda ua haulikati unaliacha likue Duka langu nilifunga biashara niliacha zote Uchumi uliyumba kwa maana nilianza pombe Niliumwa bado kidogo moyo uzime Nilimfanya ndoto kumbe naye ana ndoto nyingine Alisema anakwenda jiji la Miami Hakuna alichowaza zaidi ya kuishi kifahari Kamtumia picha na ‘mchizi’ kazikubali Na yupo tayari kumlipia gharama za safari Aliondoka na kipande kimoja cha mwili Nilikonda nilipata ugonjwa wa akili Haikuwahi kupita hata sekunde nisilie Nilitamani mpaka ardhi ipasuke niingie “JANE ALIPOONDOKA ALIMWACHIA JOHN KIDONDA KILICHOCHELEWA SANA KUPONA NA YEYE AKAWEKA NADHIRI YA KUTOJIHUSISHA NA MAPENZI TENA MAISHANI MWAKE. ALIKAA KWA MUDA MREFU BILA MAHUSIANO. LAKINI… HAKUNA DAKTARI MZURI KAMA MUDA, JOHN ALIPONA MAUMIVU NA ALIIRUDIA HALI YAKE YA KAWAIDA” Ah! Muda ukaenda nitapata ‘Mwanamwali’ Nikamwomba awe mwenza wa maisha akakubali Nikamvisha pete nikalipia mahari Sikumpenda lakini nilijifunza kumjali Aliuliza kama nampenda, nilimjibu Sikutaka kuweka moyo wake maumivu Sikutaka kuuweka Mtima wake solemba Kiasi aseme hatakuja kupenda ‘‘forever’’ Ah alinikumbatia nikamfunga kwa ishara Akanikabidhi tunda nikala Akaniamini tukajuana nikapanga kumwoa Akaidhisha na tukaanza na mipango ya ndoa “WAKATI KARNE YA 21 INAINGIA, JOHN ALIKUWA NI MIONGONI MWA VIJANA WALIOKUWA ‘FASCINATED’ NA UKUAJI WA TEKNOLOJIA YA MITANDAO YA KIJAMII. ALIJIUNGA NA DUNIA HII MPYA, MARA KADHAA ALIKAA KWENYE UBARAZA, AKIANGAZA SIMU YAKE. AKIPAPASA KILA KITUFE, NDIPO SIKU MOJA AKAPATA UJUMBE KUTOKA KWA JANE” “Habari naamini u bukheri wa afya Unaendeleaje maisha na huyo mpenzi wa sasa .nashukuru nahema ughaibuni si kwema Nakiona cha mtema mpaka naona ni heri nikafa… Ah! Maisha niliyowaza yote ni uongo Nauzishwa madawa nalazimishwa ngono Nafungiwa ndani kama mtumwa ufungwani Roho yangu rehani kiasi sasa naitamani Bongo Ukubwa umekuja kunisafisha jicho Ndoto imeisha na taswira imenionyesha sivyo, ah Naomba unifate uniondoshe kwenye hichi kifo Na hii namba ya msamaria atakueleza nilipo” Sherehe ilikuwa na mipango madhubuti Kabla mimi kuichukua michango ya Harusi Nikatoroka ughaibuni kufuata hisia zangu Kwenda kumfata njiwa wangu mahususi Nilivuka majangwa na majabali Sehemu ya safari anga sehemu nyingine bahari Niliacha kila kitu nyuma upendo na huruma vilinijaa Penzi likanipeleka mbali “JOHN ALIFIKA UGHAIBUNI, AKAMTAFUTA MSAMARIA ALIYETAMBULISHWA NA UJUMBE, MSAMARIA AKAMWELEKEZA NJIWA WAKE ALIPO, NA NIKWELI… HAPAKUWA PEMA” Nikakutana na bopa la kizungu Lenye sura ya kuichachisha mboga kwenye chungu Kiko kwenye mdomo,Tatuu kila kona na wapambe Pamoja na vishoka wenye mtutu Sio siri alizungukwa na wasichana wengi Sikujua umri walikuwa wadogo ka’ “madent” Baadhi walikuwa uchi wanahesabia “chenchi” Wengine masaji huku wengine wanamchezea nyeti “MASIKINI JOHN, ALIDANGANYA KWA KUJITAMBULISHA KAMA KAKA KWA JANE, AKIMSIHI YULE MAFIA AMRUHUSU AONDOKE NA JANE WAKAANZE MAISHA MAPYA, LAKINI… PALIPOSHINDWA SHOKA WEMBE HAUWEZI TAMBA. KWA KUZIDIWA NA UOGA WA KUUAWA… JANE ALIMKANA JOHN KWA KUSEMA HAMJUI…” Hata nilipomuuliza kama ananipenda hakujibu Akaweka moyo wangu maumivu Nilijua hawezi kufa kwa sababu hakunipenda Na ni rasmi nikapoteza shilingi kwenye msitu Nilikiambia kifo kama unakuja njoo Maana sikuwa mtu ilishakufa roho Sikuumia kama alivyoniumiza yeye Kwahiyo sikujali jinsi nilivyoteswa na wale mbwa no Aliambiwa ambusu bosi hakubisha Alipewa bunduki hakusita Aliishika risasi akaiingiza Akaambiwa anipige kwenye kichwa JOHN ALIKUWA NI JINA JIPYA LA WAHANGA WA UPENDO WA DHATI, VIPOFU WA MAPENZI, WAJINGA WA MAHABA... JOHN ALIKUWA ROMEO KWENYE ROMEO AND JULIETH, ALIKUWA SAMSON KWA DELILAH KWENYE WAHUKUMU WA AGANO LA KALE, ALIKUWA JACK KWENYE TITANIC, FRED WEASLEY KWENYE HARRY POTTER.. JOHN ALITUKUMBUSHA KUWA UPENDO NI SADAKA, SADAKA YA MUDA NA PESA, ALITUKUMBUSHA UPENDO NI SADAKA YA DAMU JOHN, ALIPOTEZA UHAI AKIWA KWENYE SAFARI YA KUTAFUTA UPENDO WA MTU ALIYEMHUSUDU NA JANE ALIPOTEZA AMANI NA THAMANI YAKE KAMA MTU AKIWA KWENYE SAFARI YA KUTAFUTA UTAJIRI ALIOUHUSUDU Hatia iko wapi?
@challymchaff3743 жыл бұрын
Daaah dizasta wewe ni vina hivi naanzaje kuchoka kusikiliza nyimbo zako
@wilsontonga37283 жыл бұрын
🤝🏾
@dullywamashairi1213 жыл бұрын
Naskiza ngoma mpaka moyo unataka kupasuka. Dizasta vina, MC Mahiri, Mc Katiri. Yaan hauishi kbs katika dunia tunayoishi sisi! Huku kwetu kitaa kizima wanajua n kiasi gani Mwamba unawika, wameacha kuniita jina langu, sikuhizi wananiita Dizasta Vina. Ngoma zako ni ngumu, mtu akiziskiliza sana lazima awe Jasiri, awe katiri na hana hatia. Ngoma zako zinaweza kumfanya mtu akatishe ktk msitu mnene wenye kutisha na asiogope. Ngoma zako zinamfanya mtu ajifunze kuwa mwenye maamuzi magumu bila kuhofia lawama la mwenye kulaumu! Dizasta vina, katika ulimwengu wa Hip Hop zaidi yako wewe bado sijamuona mwingine. Hata Fareed Qubanda umemtupa kule, kabakia jina tu! Hebu pitia hii ili uone uzao wa tungo zako broo kzbin.info/www/bejne/laeqpmeiZrKig9k
@castorymwaipopo2903 жыл бұрын
Nakukubali sana bro 💪
@sautidawa22223 жыл бұрын
Real talent
@emilysaimon4813 жыл бұрын
Dizasta vina bro we ni mkaliii Sikumpenda lakini nilijifunza kumjali Kama tupo pamoja tia like 25-12-2020
@dizastavina3 жыл бұрын
Thanks.. Please share. Usisahau kuorder my new album
@emilysaimon4813 жыл бұрын
@@dizastavina pamoja bro nigei no yako
@dizastavina3 жыл бұрын
@@emilysaimon481 pre order kupitia tigo pesa 0655696811 au Mpesa 0762158871
@msolidwagalilaya60946 ай бұрын
Brother ushaandika HATIA nyingi sana lakini hii hatia IV ni funga kazi brother
@shabannyamsalika3 жыл бұрын
Hii ngoma ni zaidi ya albamu nzima ya Weusi, Prof Tungo we ni 🔥🔥🔥🔥🔥
@dullywamashairi1213 жыл бұрын
Ngoma zake ni ngumu, mtu akiziskiliza sana lazima awe Jasiri, awe katiri asiye na hatia. Hebu pitia na hii link ili uone video, ni kitu kilekile ila mapishi tofauti. Haya ni mambo ya kutisha kzbin.info/www/bejne/laeqpmeiZrKig9k
@shabannyamsalika3 жыл бұрын
@@dullywamashairi121 Hip hop inahitaj wenye uwezo mkubwa wa kufkr, pole sana kwako mwny uwezo mdogo nkushauri kasikilize waaah!!!
@dullywamashairi1213 жыл бұрын
@@shabannyamsalika inaelekea wewe ndo hujanielewa Mimi. Wewe bado mbana pua. Wagumu wakipita wataelewa nimemaanisha nini. Umekurupuka mzee, maana kitaani wamenibatiza jina wananiita Dizasta vina!!💪💪💪
@shabannyamsalika3 жыл бұрын
@@dullywamashairi121 We ndo umekurupuka kusema huu wimbo ni wawagumu, hii ngoma anasikiliza mtu yeyote na anaelewa. Tuondoe mawazo finyu ya kudhania kuwa hip hop inasikilizwa na watu wagumu, cjui makatiri km wewe ulivyosema mwanzo...
@obeidjoseph36103 жыл бұрын
@@dullywamashairi121 mwanangu ww bado Sana na hilo jina la dizasta mwalichafua kitaan kwenu
@camillomakongwa83083 жыл бұрын
This dude is a script writer, story teller inshort ni Verteller,,, he can compose a movies of 2 hrs in 7 mins,, daaaamn🔥🔥🔥🔥
@dizastavina3 жыл бұрын
Thanks, please share
@dullywamashairi1213 жыл бұрын
Ngoma zake ni ngumu, mtu akiziskiliza sana lazima awe Jasiri, awe katiri asiye na hatia. Hebu pitia na hii link ili uone video, ni kitu kilekile ila mapishi tofauti. Haya ni mambo ya kutisha kzbin.info/www/bejne/laeqpmeiZrKig9k
@mussabutanwa86933 жыл бұрын
@@dullywamashairi121 yes he's a genius we should support him lol!!!
@dullywamashairi1213 жыл бұрын
@@mussabutanwa8693 dats true my blood Dizasta vina: The man one army 💪💪
@mussabutanwa86933 жыл бұрын
@@dullywamashairi121 yes for really man
@wawesttv9 ай бұрын
... nilipo mwambia nampenda hakujibu... 2024
@maishacenter-eastafricatv39763 жыл бұрын
Duuhh nlichelewa😪😪😪 Dizzasta's fan number one from +257🇧🇮🇧🇮🇧🇮
@ashuramuhammed3257 Жыл бұрын
Dizasta hii nyimbo ni funzo tosha yani ww ndo mwalimu wangu najifunza vitu vingi nkasikiliza nyimbo zako$
@winfredykahwili15133 жыл бұрын
Huu mziki wako ni dawa ya ubongo asee Viva dizasta vina 💪💪💪👊👊💥💥💥
@louiskhan73723 жыл бұрын
Hii True story nimesikiza ×10....song imenipeleka mpaka gaibuni ....utahisi mkono wa mungu umeandika Hii✔✔#KingOfRap
@tiktoktv86783 жыл бұрын
Wasanii kama hawa Bongo ni wachache Sana... Big up bro....
@yusuphmyinga28 күн бұрын
2024 Tunard kula madin kwa mwamba Ngoma hazichoshi vina Zawad yetu wapenda hip hop🙏
@kelvinshayo6083 жыл бұрын
Nilikwambia unajua na ctoacha kukwambia unajua💪💪
@dizastavina3 жыл бұрын
Thanks kev
@ARUSHA_NAILS3 жыл бұрын
Dah dizasta umezigusa hisia umenifanya nijione mwenye hatia
@erastompongo84003 жыл бұрын
Dah Kama umeniimba mimi vile Haso za mapenzi duniani zinaumiza wengi
@jamesngadaya27913 жыл бұрын
dizasta unao uwezo mkubwa sana wenye nguvu kama meli ya mizigo aiseee
@legawayz60933 жыл бұрын
Hii ni movie kabisa bro one day andaa scripts then simama as diirector naamini itakuwa kazi kubwa BIG UP DIZASTA VINA
@dizastavina3 жыл бұрын
Hopefully one day
@BabaNasritz Жыл бұрын
naikubali kinoma hingoma bigp bro
@aloycemaembe81163 жыл бұрын
Nmekubar bro salut kwa hii kaz
@nassoroally60933 жыл бұрын
Bro kuna haja sanaa yako ifike ktk jamii na ipigwe promo.. Kuna ujumbe madhubuti
@jeovangisc79573 жыл бұрын
Daaaa bro unajua mpaka unaboa.. masikio yetu hayalali njaa kila unaposhika kipaza!!
@benyvoice94153 жыл бұрын
Kaka hii ngoma naomba niifanyie cover yn nmeikubal Kias kwmb mpk nawaboa watu Everyday nackiliza
@michaelmasanja63433 жыл бұрын
Verteller ...Dah huwezi amini nimeiona movie yote kichwani mwangu the way Mwamba unavoflow... nilichofeli ni kuipata sura ya Jane.
@alextanzania3 жыл бұрын
Dizasta vina ni akina Joh 70. Mtiririko mzuri ,kazi nzuri. Big up brother.
@raymondtsumah64107 ай бұрын
Ogopa mwanamke💔
@ibuibu52473 жыл бұрын
jamaa lnajua sanaaa .....
@peterbenjaminpeterbenjamin95663 жыл бұрын
Aisee dizastar noma Sana mshkaji wangu darasa Hilo namimi napenda Nije nipate mautundu ya asali ya hip-hop
@salehekasangas3291 Жыл бұрын
Umeshushwa.brooo...yan.unajuaa.brooo
@bonnifacewilly30263 жыл бұрын
Daaah huyu jamaa anafanya mziki kwa bongo hakuna tena kama dizasta amani kwako brother
@aaronjohn95183 жыл бұрын
Deep sana hii ni kama movie
@mwajumakarim85203 жыл бұрын
Wewe wewe weeeeeewe🥺🥺🥺ulishushwa ututeke🇹🇿❤️
@dullywamashairi1213 жыл бұрын
Ngoma zake ni ngumu, mtu akiziskiliza sana lazima awe Jasiri, awe katiri asiye na hatia. Hebu pitia na hii link ili uone video, ni kitu kilekile ila mapishi tofauti. Haya ni mambo ya kutisha kzbin.info/www/bejne/laeqpmeiZrKig9k
@rachelgmartin68503 жыл бұрын
Sauti yako tu mi hoiiiii🙆🏻♀️🙆🏻♀️🙆🏻♀️🙆🏻♀️🙆🏻♀️🙆🏻♀️🙆🏻♀️🙆🏻♀️🌹🥰❤️
@dizastavina3 жыл бұрын
Thank you........
@learntoearn95883 жыл бұрын
Muda utafika Inshaallah dizasta utakua jina kubwa na ramani ya maarifa kwa kizazi kijacho
@dizastavina3 жыл бұрын
Hopefully
@emmabelljohn40863 жыл бұрын
Nomaa sanaa
@hollymore49043 жыл бұрын
We jamaa. Kuna tamaduni music na Kuna dizasta music... Hakika. Hii sio tamaduni,hii dizasta
@danchalzndyanabo92003 жыл бұрын
Dizasta vina noma sana
@obeidjoseph36103 жыл бұрын
Unatishaaa yaaaani hiii ngoma mengne live
@sabrisaleh17203 жыл бұрын
We dizasta fundi ni kweli nikitaka mziki mzuri nimtafute dizasta
@danielmalimi98903 жыл бұрын
Duuuhhh.... hii inabeba sababu muhimu ya muziki kwenye maisha....
@revocatuscharles1512 Жыл бұрын
Jamaa unaimba sana aiseh🔥🔥🔥🔥
@chibalevicent822 Жыл бұрын
You are so Genius, asante kwa uwezo wako wa kunifanya niamini kuwa wewe ndie Rapper Bora
@claudekeverenge44043 жыл бұрын
Oyaah Vina wewe sio wa sayari hii hii umeuwaa.. Hii ndio hip hop
@dizastavina3 жыл бұрын
Thanks bro
@kibafteshadau222 Жыл бұрын
Yule dogo raptcha akae mbali....ajifunze kuchana, sio fujo nyingi ....dizasta ni disaster balaa🔥
@furahinandrew97043 жыл бұрын
We jamaa nomaa
@boygavana46743 жыл бұрын
Dizasta ww sio binadamu wa kawaida aseee haijawahi tokea
@deviceboykifaa59853 жыл бұрын
nakubali yan huja wahi ikosea nafis yangu kak
@brainfigure943 жыл бұрын
Dizasta vina saiv umesha convert akili yangu kwenye hiphop naenjoy sana napo usikia mziki wako nakuwa makini ili nielew unachokimaanisha nanukuu kwenye hatia 2 ulisema wanaume wote mbwa ila cjui sasa wewe ni kubwa la ma mbwa mana sioni wa kucompare na mziki unaoimba
@dizastavina3 жыл бұрын
Shukrani sana ndugu, please share na marafiki
@Tobey1988ful3 жыл бұрын
New fan from +254 hapa.... Huyu kaka balaa sanaa dah
@dullyhaleem69622 жыл бұрын
Hii nyimbo itungiwe movie kummmke duuh😓😓🔥🔥🔥
@johnkerrysibomana90622 жыл бұрын
Nimerudi hapa baada ya mistari mingi kunigusa na kuendana na ninachikipitia kwenye maisha ya mahusiano
@oscarsospeter80342 жыл бұрын
Wewe ni mtunzi Huru Dizasta vina God Abless njia zako
@hassanihanzel3 жыл бұрын
Wa KUMI kutazama 🙌
@dizastavina3 жыл бұрын
👏🏾 👏🏾 👏🏾 👏🏾
@KelvinEmersonSteven3 жыл бұрын
Aisee hii ni ya moto kushinda jua🔥🔥🔥🔥
@dullywamashairi1213 жыл бұрын
Ngoma zake ni ngumu, mtu akiziskiliza sana lazima awe Jasiri, awe katiri asiye na hatia. Hebu pitia na hii link ili uone video, ni kitu kilekile ila mapishi tofauti. Haya ni mambo ya kutisha kzbin.info/www/bejne/laeqpmeiZrKig9k
@rashidynnungu67753 жыл бұрын
we jamaa unajua shikamoo sana
@dizastavina3 жыл бұрын
Marahaba 😎 😎 😎
@sayeedally81523 жыл бұрын
kazi nzuri bro,,,, nakubali kazi zakoo
@meshack25593 жыл бұрын
Mistar unachora Broo!!! Ni nomah ,we mkali aise,big up
@binyezanch82713 жыл бұрын
Wimbo wangu wa mwaka kbsa Asante dizasta 2020
@dizastavina3 жыл бұрын
Apreciate, umeshaweka order ya album
@awetubello53993 жыл бұрын
Brother unawezaaaaah na xo unaweza 2 we ni MWALIMU
@dizastavina3 жыл бұрын
Thanks bro
@novatusanthony85633 жыл бұрын
Hii goma inatakiwa wasambaziwe wanafunzi Tanzania mzima maana hili ni somo linajitegemea.
@valentinesyekeye6846 Жыл бұрын
Upewe maua yako mzee. Hizi ni zaidi ya tungo
@saimonkimolo53136 ай бұрын
Dah broda kila siku nasikilza hii ngoma tangu itoke nimwaka watatu huu story flan ilionitokea kabsa lakn si mbele hapahapa bongo
@directorluganongonya72123 жыл бұрын
Daaah ! Shikamoo tena
@dizastavina3 жыл бұрын
🙏🏼🙏🏼
@kelvinmzopola51863 жыл бұрын
Daaaaah so sad 😌 ila we jamaa unajua kinoma
@saidamour26353 жыл бұрын
Disasta unaweza sana amini wanakuelewa ila wanabana tu, fans wako tunasubri collabo yako na kaa la moto.
@jumangala Жыл бұрын
Ausio
@nelsonkedmon85343 жыл бұрын
Nakubali sana hujawahi kosea the vertller
@dullywamashairi1213 жыл бұрын
Ngoma zake ni ngumu, mtu akiziskiliza sana lazima awe Jasiri, awe katiri asiye na hatia. Hebu pitia na hii link ili uone video, ni kitu kilekile ila mapishi tofauti. Haya ni mambo ya kutisha💪💪 kzbin.info/www/bejne/laeqpmeiZrKig9k
@erickpaschaljr86673 жыл бұрын
Ahsante sana Dizasta Vina Kwa Muziki Mzuri unaoacha/utakaoacha Alama ya Milele
@fundi_nyata3 жыл бұрын
THE VERTELLER!! Wachache watakuelewa na kukusifia!!
@gideonaire_ke3 жыл бұрын
kazi safi sana Dizasta
@dizastavina3 жыл бұрын
Sijaona order yako brother?
@gideonaire_ke3 жыл бұрын
@@dizastavina order ya nini bro?
@dizastavina3 жыл бұрын
@@gideonaire_ke the Verteller ALBUM.. Coming up this Sunday
@kangeyg68793 жыл бұрын
Master vina fan toka 🇰🇪🔥✅ tumengoja sana umewakilisha kama kawaida
@dizastavina3 жыл бұрын
Thanks, please share
@mosesbond2023 жыл бұрын
Wewe mwamba ni mwehu sema tuu unafikiri sana Yaani movie moja classic
@dizastavina3 жыл бұрын
😂 😂 😂
@johnmosha82853 жыл бұрын
Makini sana mzee
@jofreymfugale47523 жыл бұрын
Aliondoka na kiungo cha mwili 😃🔥🔥
@IddyKatyawa2 ай бұрын
Umetisha
@richardtitus85393 жыл бұрын
Daaah black maradona.. home boy unajua
@mwajumakarim85203 жыл бұрын
Nakuona mbali
@dullywamashairi1213 жыл бұрын
Naskiza ngoma mpaka moyo unataka kupasuka. Dizasta vina, MC Mahiri, Mc Katiri. Yaan hauishi kbs katika dunia tunayoishi sisi! Huku kwetu kitaa kizima wanajua n kiasi gani Mwamba unawika, wameacha kuniita jina langu, sikuhizi wananiita Dizasta Vina. Ngoma zako ni ngumu, mtu akiziskiliza sana lazima awe Jasiri, awe katiri na hana hatia. Ngoma zako zinaweza kumfanya mtu akatishe ktk msitu mnene wenye kutisha na asiogope. Ngoma zako zinamfanya mtu ajifunze kuwa mwenye maamuzi magumu bila kuhofia lawama la mwenye kulaumu! Dizasta vina, katika ulimwengu wa Hip Hop zaidi yako wewe bado sijamuona mwingine. Hata Fareed Qubanda umemtupa kule, kabakia jina tu! Hebu pitia hii ili uone uzao wa tungo zako broo kzbin.info/www/bejne/laeqpmeiZrKig9k
@RamaSwalehe-kc9kr Жыл бұрын
Unyama sana broo
@tinnohaugustineh61939 ай бұрын
Vina vingi sana humu👑
@octavianmushi9283 жыл бұрын
Brazaaa umegusa maisha ye2 kwa hii ngoma
@nashonshimba79973 жыл бұрын
Imenitoa machoz hii ngoma mapenz yanauma sana
@dullywamashairi1213 жыл бұрын
Ngoma zake ni ngumu, mtu akiziskiliza sana lazima awe Jasiri, awe katiri asiye na hatia. Hebu pitia na hii link ili uone video, ni kitu kilekile ila mapishi tofauti. Haya ni mambo ya kutisha kzbin.info/www/bejne/laeqpmeiZrKig9k
@ramadhanally1383 жыл бұрын
My broo really umenitoa mazur kweli VINA NI HAFAHI KABISA
@josephcanizio3 ай бұрын
Muziki unaishi na unajenga na kuponya hakika hii ni dawa kwenye kufkiria kabla ya kutenda❤❤🧠
@shaybumpala20623 жыл бұрын
Daaah We Ni Zaidi ya Binadamu Tulosimuliwa Vitabuni 🤔🤔🤔 Wewe ni Nani Unajua Kinoma Noma Sanaa Imeshibishwa Kabissah
@dizastavina3 жыл бұрын
Appreciate the love brother. Please share
@ommymsomi43623 жыл бұрын
Ningekua baraza la sanaa ngomaa zako kaka zingetumika kujibia mitihan kaka...yan wanafunz ningewataka waskize kisha wachambue kila kipengele cha fasihiiiiiii
@lonely86823 жыл бұрын
Najivunia kua shabiki ako bro...hujawahi kuniangusha🙏🙏🙏🙏🔥🔥🔥🔥
@dullywamashairi1213 жыл бұрын
Ngoma zake ni ngumu, mtu akiziskiliza sana lazima awe Jasiri, awe katiri asiye na hatia. Hebu pitia na hii link ili uone video, ni kitu kilekile ila mapishi tofauti. Haya ni mambo ya kutisha kzbin.info/www/bejne/laeqpmeiZrKig9k
@GerrardTryphorn4 ай бұрын
Daaa hiingom Kali
@ombenedwin1363 жыл бұрын
Mungu ametupaga disaster vina
@franciscojonja11643 жыл бұрын
Asie elewa kazi ya hiki kichwa aisee hatokuja kuelewa milele @dizasta vina ndio nembo ya hip hop isio vunja nguzo ata moja ya hip hop brother umetisha sana
@dizastavina3 жыл бұрын
Thanks, please share
@balikiabdala823 Жыл бұрын
🤔🤔🤔🤔 Noma sana ngoma kali sana
@brainfigure943 жыл бұрын
Kuna haja ya dizasta kufungua chuo cha mziki wa hiphop ili vizazi vinavyokuja vielewe maana ya muziki wa hiphop
@dizastavina3 жыл бұрын
👏🏾 👏🏾 👏🏾 👏🏾
@sylvestermtweve28953 жыл бұрын
Dizasta..... you're very UNIQUE broo...Mungu akuzidishe maarifa na afya tele just because unajua kutupa Raha mashabiki zako..GOD BLESS TOUR TALENT
@dizastavina3 жыл бұрын
Thanks bro
@vigangwaya88023 жыл бұрын
The best hiphop rapper kwa sasa nchini, hakuna wa kumzidi Dizasta vina kwa sasa
@boniphacelutusyo91102 жыл бұрын
Hip hop 👍👍👍
@Mchora_tz3 жыл бұрын
Dizasta we jamaa ni hatarii no kiki no kelele ila mtaani unaleta kile tunachohitaji yaan hip hop ingekuwa hv labda tungeongea mengine mtaani #sioni km una ngoma mbovu
@dizastavina3 жыл бұрын
Appreciate, please share
@geofreymboyelwa6142 жыл бұрын
Nyimbo nzur sana
@allymarumbo10883 жыл бұрын
What a lesson..daaaaaah We jamaa ni zaidi ya hip hop bro.
@ernestmajula51433 жыл бұрын
Dizasta ✌.. Mnyama mkali
@rehemaevans752 жыл бұрын
Dizasta unajuwa bro nataman one day nikuone
@hon-mlenga3 ай бұрын
🎶🎶🎶🎶Dizasta nadownlod nyimbo zako zote
@vandiddyy57333 жыл бұрын
Duuh..! sijui nikupe jina gani broh... una hatari kubwa sana. 🙌🙌🙌
@dizastavina3 жыл бұрын
👏🏼👏🏼
@robifilosomaniofficialonli42723 жыл бұрын
Waaaaaah... Dizasta vina..tisha sana.. Kenya tunakuaminia.