Рет қаралды 416
Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Emmanuel Nchimbi amemuelekeza Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Nchemba kuiwezesha Wizara ya Ujenzi kiasi cha Shilingi Bilioni 1.8 kwa ajili ya malipo ya fidia kwa wananchi waliopisha mradi wa upanuzi wa njia nne wa barabara ya Bukoba Mjini kuanzia Rwamishenye Roundabout hadi Stendi Mpya ya Bukoba Mjini (km 1.2) ambao utekelezaji wake unaendelea.
Dkt. Nchimbi ametoa maelekezo hayo Mkoani Kagera wakati akizungumza na wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika Bukoba Mjini ambapo pamoja na mambo mengine amesikiliza na kutatua kero mbalimbali zilizotolewa na wananchi.
#wizarayaujenzi