Рет қаралды 1,408
#ikulumawasiliano #ikuluzanzibar #ccm #samiasuluhuhassan #habarimaelezo #ktnnews #wizarayahabari #wizarayakilimo#tanzania
TANZANIA inatarajiwa kuwa mwenyeji wa mkutano wa masuala ya nishati barani Afrika utakaotafuta namna ya kukusanya dola za Marekani bilioni 190 ili zitumike kufikisha umeme kwa wananchi milioni 300 barani humo ifikapo mwaka 2030.
Hatua hiyo inatokana na mkakati wa Serikali ya awamu ya sita kupeleka umeme vijijini na vitongojini kwa kasi hali ambayo imezivutia taasisi za Benki ya Dunia na Benki ya Maendeleo Afrika (AfDB) kuamua kufanya mkutano huo mkubwa ifikapo Januari, 2025.
“Wameridhishwa na utendaji kwenye sekta ya nishati, wameridhishwa na mkakati wa Serikali wa kupeleka umeme mpaka vijijini, siyo tu vijijini lakini mpaka kwenye kila nyumba. Wameamua kuitisha mkutano mkubwa barani Afrika ambao utawakutanisha wadau mbalimbali, taasisi za Kimataifa na taasisi zinazotoa mikopo kwa wajasiriamali na makampuni ili waweze kuwekeza kwenye umeme.”
Hayo yamesemwa na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa kwenye mkutano wa kujadili ajenda ya upatikanaji wa nishati Afrika ulioandaliwa na taasisi ya Global Energy Alliance for People and Planet (GEAPP) jijini New York, Marekani.
Follow us on:
FACEBOOK;
SpotiLeo: / spotileo-176. .
HabariLeo: / habarileo
DailyNews: / dailynewstz
INSTAGRAM;
HabariLeo: ....
SpotiLeo: ....
TWITTER;
Twitter HabariLeo: Ha...