Рет қаралды 77,965
Siku moja baada ya kuzikwa kwa Mjumbe wa Sekretarieti ya Chadema Ally Mohamed Kibao aliyetekwa kwenye basi la Kampuni ya Tashriff na kuuwawa,Msimamizi wa mabasi hayo Dar es Salaam Shabani Shemweta amesema wanaendelea kutoa ushirikiano kwa Jeshi la Polisi kuwatambua wahusika waliomuua kada huyo.
Amesema mtu mmoja aliyekuwa msafiri ambaye alijumuika na watekaji alitoa alijitambulisha kwa jina la Bakari.
Kibao aliyetekwa Septemba 6,2024 eneo la Kibo Complex Tegeta jijini Dar es Salaam akiwa kwenye basi la Tashriff akielekea Tanga.
Inaelezwa basi hilo lilisimamishwa na watu waliokuwa kwenye magari mawili mbele na nyuma,watu wawili wakiwa na silaha za moto wakiingia ndani ya gari kumkamata mzee huyo huku mmoja akienda mbele ya basi na kumuamuru dereva asiondoe basi.
Septemba 7,2014 Katibu Mkuu wa Chadema John Mnyika alitangaza kutokea kwa tukio hilo kabla ya Septemba 8,2024 mwili wa Ally KIbao kuokotwa Ununio Dar es Salaam na kuupeleka Hospitali ya Mwananyamala.
Baada ya utambuzi wa mwili wa mzee huyo aliye mwagiwa tindikali usoni na kusababishiwa majeraha mengine,
Siku hiyo hiyo Jeshi la Polisi kupitia taarifa yake kwa umma limesema tayari uchunguzi wa tukio hilo umeanza huku ukiwakaribisha wenye ushahidi wa tukio hilo kushirikiana na Polisi