Рет қаралды 35,145
Moshi. Familia ya Ephagro Msele, mfanyabiashara anayedaiwa kuuawa na mkewe inajiandaa kwa maziko baada ya hatua uchunguzi wa Polisi kukamilika na kukabidhiwa mwili.
Msele anadaiwa kuuawa kwa kuchomwa kisu mgongoni na mkewe, Beatrice Elias, Mei 25, mwaka huu, katika tukio linalohusishwa na wivu wa mapenzi.
Kulingana na taarifa za Polisi, Msele alikuwa nyumbani kwa mzazi mwenzake wakati Beatrice alipomvizia na kumshambulia.
Polisi wamemkamata Beatrice kwa tuhuma za mauaji na anashikiliwa huku uchunguzi ukiendelea.
Akizungumza na waandishi wa habari leo, Mei 27, ndugu wa marehemu, Philip Msele, amesema tayari familia imepokea mwili wa ndugu yao baada ya uchunguzi wa kitabibu katika Hospitali Rufaa ya KCMC na sasa inakutana kupanga ratiba na taratibu za maziko.
Maziko ya Msele yanatarajiwa kufanyika hivi karibuni kwenye eneo la familia.