Рет қаралды 29,002
Mtoto wa msanii Nurdin Bilal maarufu kama 'Shetta' Qailah Nurdin Bilal amechaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Chipukizi CCM Taifa baada ya kupata ushindi katika mkutano Mkuu wa Chipukizi Taifa.
Katika uchaguzi huo uliofanyika Desemba 20, 2023, kinyang'anyiro cha nafasi ya Mwenyekiti waliowania nafasi hiyo ni Neema Kinyonga aliyepata kura 13, John mpoto kura 17, Hytham Mwanyemba kura 96 na Qilla Nurdin akipata kura 303.
Baada ya ushindi huo Mwenyekiti Mpya wa UVCCM Chipukizi Taifa, Qailah Nurdin Bilal akapata nafasi ya kuzungumza na kuahirisha mkutano wa uchaguzi.