Рет қаралды 4
Kero ya maji katika kata ya Ruaha Mbuyuni wilayani kilolo Mkoni Iringa imeonekana ni kubwa kiasi ambacho wananchi wa eneo hilo wakilalamika kutumia maji ambayo si salama.
Hayo yamezungumzwa na baadhi ya wananchi wa kata ya Ruaha Mbuyuni wakati wakitoa kero zao mbele ya mkuu wa mkoa wa Iringa Peter Serukamba 27 Septemba 2024 wakati alipofanya ziara ya kusikiliza kero za wananchi na kusema wanatumia maji yasio salama kitu ambacho kinapelekea kupata magonjwa .
Aidha Wananchi hao wamemuomba Mkuu wa mkoa wa Iringa kufanya mpango wa maji kufika katika kituo Chao Cha afya Kwani kwa sasa Kuna baadhi ya huduma zimekuwa hazifanyiki kutokana na kuwa na uhaba wa maji.
Kwa upande wake msimamizi wa RUWASA wilayani kilolo amesema maji yanatoka machafu kwa sababu yanatoka hifadhini na huko Kuna wanyama lakini wameshaagiza chujio kwa ajili ya kuchuja maji hayo
Katika kutatua kero hiyo Mkuu wa Mkoa wa Iringa Mhe. Peter Serukamba amemuagiza Mkurugenzi wa Halmashuri ya Wilaya ya Kilolo, kupitia mapato ya ndani kutenga fedha kwaajili ya ununuzi wa Chujio ili wananchi kutoka Kata ya Ruaha Mbuyuni waweze kupata Maji safi na salama.
Aidha Mkuu wa mkoa wa Iringa Peter Serukamba amesema Serikali inaaleta pesa nyingi kwajili ya shuhuli za maendeleo kwa wananchi wake kwani wananchi hao wanalipa Kodi hivyo kuhusu maji safi na salama watapata kwani chujio lipo njiani kufika.
#nurufm #nurudigital