Рет қаралды 89
Wananchi wa Mtaa wa Chikowa Kata ya Mbabala Jijini Dodoma wameiomba Serikali kutowaondoa katika eneo wanaloishi kwa madai ni mali yao lakini ikihitaji walipwe fidia.
Madai hayo yamekuja baada ya Serikali kupeleka tangazo la kuwataka wahame kwenye kupisha ardhi hiyo ambayo imepangiwa matumizi mengine ya Serikali tangu ilipokuwa Mamlaka ya Ustawishaji Makao Makuu Dodoma (CDA).
Hata hivyo Mkuu wa wilaya ya Dodoma Alhaj Jabil Shekimweri amesema ardhi hiyo ilichukuliwa kisheria kwa ajili ya matumizi ya Serikali lakini akaomba wananchi kama wanaona iko haja waende mahakamani ili kutafuta haki yao.