Рет қаралды 17,515
Luka 15:11-19
Wengi tunamuangalia shetani katika upande wa kuchelewesha vitu,lakini tunasahau kwamba kuna wakati shetani huwahisha vitu na kutokana na hilo akakuharibia maisha yako.
Ukisoma mstari wa 11-12 tunaona yule mtoto mdogo ndio alitaka urithi.Kiuhalisia mtu anayetoa urithi ni yule ambaye yuko karibia na kufa,kwahiyo alipotaka urithi kabla baba yake hajafa kuna eneo ambalo aliliua kwa baba yake,eneo la maamuzi.Ndio maana huoni baba yake akibisha,na hakuishia hapo tu bali aliwapa urithi watoto wake wote wawili hata yule ambaye hakuomba.
Mstari wa 13 unasema;
Luka 15:13
[13]Hata baada ya siku si nyingi, yule mdogo akakusanya vyote, akasafiri kwenda nchi ya mbali; akatapanya mali zake huko kwa maisha ya uasherati.
Baada ya huyu mtoto mdogo kupewa tu urithi wake hakukaa sana,alichukua vitu vyote alivyopewa na akaenda nchi ya mbali kabisa.Kuwa makini sana ukiona jambo linakusukuma usiwe na subira,chunguza kujua ni kitu gani kinakusukuma ufanye maamuzi ya haraka hivyo.Shetani alihakikisha huyu mtoto anaenda mbali kabisa na uwepo wa baba yake.Adui anapotaka kukupiga lazima kwanza akutengenezee mazingira ya kujitenga na anakupa kabisa na sababu za msingi.
UNAWEZA WASILIANA NASI AU KUTUMA SADAKA YAKO KWA NAMBA HII : 0657 173 322
Unaweza kutufuatilia katika mitandao yetu ya kijamii
Like our Facebook: / therealityof. .
Follow our Instagram: / realityofch. .
Subscribe our KZbin: kzbin.info/door/67L...
Also Subscribe Roc worshippers youtube channel: / @rocworshipperz
#Sunbellakyando #RealityofChrist #Rocmedia