Рет қаралды 2,762
Wakati abiria wanaotumia bandari ya Dar es Salaam kwenda Zanzibar na kurudi Dar wakilalamikia foleni katika eneo la ukaguzi hatua inayosababisha wachelewa katika maeneo wanayokwenda hasa baada ya kufika Dar es Salaam wakitokea Unguja, Uongozi wa Bandari ya Dar es Salaam, umesema upo mbioni kulifumua na kuliboresha eneo linalotumiwa na abiria (Baggage room).
Wakizugumza na Mwananchi Digital abiria hao wamesema mbali na kupoteza muda wakiwa bandarini pia wamekuwa wakikosa mabasi yaendayo mikoani.
Mkurugenzi wa bandari ya Dar es Salaam, Mrisho Mrisho katika mahojiano maalumu na Mwananchi Digital amesema wamekusudia kufanya ukarabati mkubwa katika gati hiyo ili kuondoa changamoto kwa abiriakuhusu mikakati mbalimbali ya taasisi yake ikiwemo changamoto zinazoikumba ‘Baggage room’.