Рет қаралды 10,909
Bunge limepitisha azimio la kuondoa kigezo cha kupitia mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) pamoja na Jeshi la Kujenga Uchumi (JKU) kwa vijana wanaoomba nafasi za ajira katika vyombo vya ulinzi na usalama.
Azimio hilo limekuja kufuatia hoja ya dharura iliyotolewa jana Alhamis Februari 15, 2024 na Mbunge wa Mbozi, George Mwenisongole na kisha Spika wa Bunge, Dk Tulia Ackson kutaka kujiridhisha ikiwa Bunge limeshawahi kutoa maelekezo juu ya jambi hilo.
Hata hivyo baada ya kujiridhisha kuwa hakukuwahi kuwa na maelekezo juu ya jambo hilo alimruhusu Mbunge huyo kutoa hoja ambayo iliungwa mkono na kisha ikajadiliwa na azimio likatoka.
Hata hivyo wakati akitoa hoja ya kuahirisha Bunge Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa alilitaja azimio kupitishwa na Bunge kama moja ya maazimio yaliyopitishwa kwenye mkutano huu wa Bunge.