Рет қаралды 12,908
Mbunge wa Kisesa, Luhaga Mpina ametaka Bunge limtake Waziri Mkuu awafukuze kazi wizara nzima ya Maliasili na Utalii kuanzia waziri mpaka mfagiaji kwa kile alichopkiita ni kumdharau Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, maagizo ya Bunge na yeye mwenyewe.
Mpina amesema hayo leo Jumatatu, Juni 3, 2024 wakati akichangia mjadala wa makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa mwaka wa fedha 2024/25 jijini Dodoma.