Рет қаралды 41
MAKONDA, DKT. BITEKO NA AWESO KUUJADILI MRADI WA MAJI WA BILIONI 520 ULIOSHINDWA KUTEKELEZEKA.
Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Paul Christian Makonda amepanga kukutana na Naibu Waziri Mkuu ambaye pia ni Waziri wa nishati nchini Tanzania Dkt. Dotto Biteko na Waziri wa maji Jumaa Aweso kujadili juu ya gharama kubwa za uendeshaji wa mradi wa maji, unaotekelezwa kwenye jiji la Arusha, maarufu kama mradi wa Bilioni 500.
Mhe. Paul Makonda amefikia hatua hiyo leo Jumamosi August 17, 2024 wakati wa kikao kazi na maafisa wa Mamlaka za Maji mkoa wa Arusha na kuwaomba uvumilivu wakazi wa jiji la Arusha wakati huu ambapo ameahidi kutafuta suluhu ya kudumu ya mradi huo wa maji.
"Hili jambo lazima tulikalie kikao na tulitafutie ufumbuzi wa haraka kwa kukubaliana kwa pamoja kwamba tuiombe Wizara yetu ya Nishati ituingize kwenye watoa huduma na tutoke kwenye Unit moja ya watu wa viwandani kuja kwenye unit moja ya watu wa makazini ili kusaidia kupunguza mzigo wa uendeshaji wa mradi huu" Ameongeza Mhe. Makonda.
Mhe. Makonda ametumia nafasi hiyo pia kuwataka wataalamu mbalimbali ndani ya mkoa wa Arusha kuongeza umakini kwenye usimamizi wa miradi hasa katika hatua zake za awali za usanifu ili kutokuwa na miradi isiyotekelezeka na yenye gharama kubwa za uendeshaji suala ambalo limekuwa likiwaumiza walengwa wa miradi hiyo ya maendeleo.