Рет қаралды 278
Mwanafunzi wa darasa la sita katika shule ya msingi Somanda 'A' wilayani ya Bariadi mkoani Simiyu, Hollo Malugu (14) ameshambuliwa na kujeruhiwa na fisi wakati akiwa anaenda shule.
Tukio hilo limetokea leo Machi 10, katika mtaa wa Izunya ambapo mama wa mtoto Mwasi Masinge Sumbuka ameeleza kuwa mtoto aliondoka nyumbani majira ya saa 12 asubuhi na baadae alisikia yowe ndipo alipotoka kutazama kinachoendelea na kukuta mtoto akiwa chini anagaa gaa.
Mganga mkuu wa hospitali ya mji wa Bariadi Judith Ringia amethibitisha kumpokea mgonjwa huyo na kusema kuwa wamempokea akiwa katika hali mbaya na kumpa huduma ya kwanza na kumpa rufaa ya kwenda hospitali ya kanda Bugando kwa ajili ya matibabu zaidi.