Рет қаралды 834
Kutokana na kushamili kwa wizi wa mifugo katika wilaya ya Bariadi mkoani Simiyu wananchi wa kata ya Nyangokolwa na Somanda wamefanikiwa kukamata kundi la Ng'ombe 54 Kondoo 3 na mbuzi 4 wanaosadikiwa kuwa ni wa wizi ambao walikuwa wanapelekwa mnadani.
Mtuhumiwa aliyekamatwa na mifugo hiyo ameeleza kuwa alikabidhiwa mifugo hiyo ili kuisafirisha kwenda mnadani huku baadhi ya waliomkabidhi akiwa anawafahamu kwa sura.