Рет қаралды 8,172
Mzinga wa kufuga Nyuki Kibiashara uliopewa jina la "SINGIDA TECHNO-HIVE" ambao ni Matokeo ya Utafiti kwa Miaka Sita(6) iliyopita. Mzinga huu unatatatua Changamoto Nyingi zinazowakabili wafugaji wa nyuki mijini na Vijijini. Mkurugenzi Mtendaji wa Kijiji Cha nyuki co Ltd amesema Kampuni imejipanga kuweka Mizinga Millioni moja kwenye Ardhi ya Tanzania ili kuongeza KASI ya Uzalishaji wa Mazao na Bidhaa za Nyuki nchini Tanzania. " Kwa Sasa Tutafungua Ofisi katika Mikoa ya Morogoro, Iringa, Arusha , Manyara , Kilimanjaro, Mwanza na Dar es salaam baada ya Ofisi ya Dodoma na Singida kuonyesha Matokeo Chanya na Kusaidia Wafugaji Wengi zaidi kuliko idadi iliyotarajiwa. Kutokana na Ongezeko la Watanzania wanaohitaji kuwekeza kwenye Ufugaji wa nyuki Kibiashara tumejipanga kujenga Viwanda vya Kutengeneza Mizinga na Kuchakata Asali ili kuimarisha Afya na Uchumi wa watanzania kwa Haraka.