Рет қаралды 9,724
Leo imetimia mwaka mmoja kamili tangu kufariki kwa aliyekuwa makamu wa rais wa kwanza wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad, katika mahojiano maalumu makamu wa sasa wa kwanza wa Zanzibar Othman Masoud Othman amemwambia mwandishi wetu Aboubakar Famau kwamba, mpaka sasa hakuna hatua kubwa iliyopigwa katika serikali ya umoja wa kitaifa kwa sababu ya kukosekana kwa utashi wa kisiasa miongoni mwa viongozi.
#bbcswahili #tanzania #zanzibar