Рет қаралды 13,765
Waamuzi 16:21
[21]Wafilisti wakamkamata, wakamng’oa macho; wakatelemka naye mpaka Gaza, wakamfunga kwa vifungo vya shaba; naye alikuwa akisaga ngano katika gereza.
Wakati wafilisti wamemkamata Samsoni kitu cha kwanza walichofanya ni kumuondolea uwezo wa kuona.Macho hukuonesha mahali unapotakiwa kwenda(maono yako),kitu ambacho shetani hufanya ni kukuzuia usiweze kuona ile hatma ambayo Mungu amekuitia.Na huwa haishii hapo,huwa anahakikisha anakutoa kabisa kwenye kusudi ambalo Mungu amekuumbia.Samsoni alikuwa na kusudi la kuwatoa wana wa Israeli katika mikono ya wafilisti,lakini kwa kuwa walimtoboa macho(kuua maono) wakamfanya awe anasaga ngano tena gerezani.
Kuna watu kazi mnazofanya sizo Mungu alizowaitia,unafanya tu kwa sababu ndio inakupa mkate wa kila siku ila huifurahii,na sio hivyo tu hata matunda ya kazi yako huyaoni.Unaweza ukawa unapata pesa nzuri sana lakini ukikaa chini na kutazama ni maendeleo gani umeyapata kutokana na pesa hizo utakuja kuona kuwa hakuna maendeleo yoyote.
Wafilisti walipomkamata Samsoni walisahau kuwa nywele zitaota tena na kile alichokipoteza kitarudi tena.Shetani alipokutesa alisahau kuwa bado hajakuziba mdomo,utaomba na Mungu atasikia.Na atakupeleka katika hatua kubwa ambayo hawakuifikiria.
Hii ni sehemu ya kwanza ya maombezi,utakapojumuika nasi katika maombezi haya kama ambavyo Mungu amewafungua hawa akakufungue na wewe pia
UNAWEZA WASILIANA NASI AU KUTUMA SADAKA YAKO KWA NAMBA HII : 0657 173 322
Unaweza kutufuatilia katika mitandao yetu ya kijamii
Like our Facebook: / therealityof. .
Follow our Instagram: / realityofch. .
Subscribe our KZbin: www.youtube.co....
Also Subscribe Roc worshippers youtube channel: / @rocworshipperz