Рет қаралды 40,714
#SalamaNa #SendTip Through MPESA #0762797291
Support us through anchor.fm/yahs...
SUBSRIBE TO OUR CHANNEL bit.ly/YahSton...
Listen our Podcast on
Spotify Link spoti.fi/2Uxr6Cm
ApplePodcast Link apple.co/2Ou1bru
GooglePodcast Link bit.ly/GoogleP...
Audiomack Link bit.ly/YahSton...
KZbin Link bit.ly/KZbinS...
Carlos Bastos aka Kalito ni moja kati ya wale binadamu ambao hawahitaji ‘kutambulishwa’ na hiyo si kwa sababu ya muonekano wake hata kidogo zaidi ni personality yake, anaongea, anachekesha, anajielewa, anajua nini cha kusema na wapi pa kusema pia. Katika watu ambao namshukuru Mungu kwa kuwafanya wawe rafiki zangu Kalito ni mmoja wapo.
Jinsi ambavyo alifika Tanzania inaweza ikakufanya ujue pia yeye ni mtu wa aina gani haswa, kutoka mwenyewe familia ambayo mtoto wa kiume ni pekee, na pengine alikua na uhakika wa kupata kila anachotaka lakini aliamua kupaki begi na kuchanja mbuga kuja hapa Tanzania. Kusema za ukweli story yake ya maisha ni ya kuamsha sana. Imagine wewe leo unatoka ulikotoka ukaenda zako pa kwenda, ukajimix kwa kuhudumia watu kwa kuwapa burudani na chakula mpaka akapata upenyo wa kufanya yake. Ni wangapi kati yetu wanaweza kufanya hivyo? Najua wengi wetu hatukuzaliwa hapa Dar es Salaam ila tumekuja tukalikita na mpaka sasa Alhamdulillah mambo yanaenda. Ila si wengi wanaweza kusema hivyo. Tunajua huchukua jasho machozi na pengine damu kufikia malengo.
So binafsi haswa nimejifunza au najifunza nini kutoka kwa rafiki yangu huyu kila siku? Cha kwanza ni kuwa MKWELI. Kama unayo unayo, kama unaweza kufanya/kufika utafanya hivyo, kama unaweza kutoa unatoa na kama huwezi UNASEMA. Naamini ndani ya moyo wangu, hiyo ni moja ya silaha kubwa sana kama unataka kufanikiwa, kama unataka MAENDELEO. Cha pili pia ambacho bado kinakaa kwenye UKWELI ni UAMINIFU. Ukikopa pesa RUDISHA maana hii itakupa nafasi ya kuweza kurudi na kukopa tena kama mambo yako yatakua bado sio sukari, sasa imagine hujarudisha na ukapata shida nyengine je utaweza kurudi kukopa tena? Vipi kama alokukopesha nae kashawaambia ma don wenzake kwamba wewe huwa hulipi? Utasogea kweli?... Mwisho wa siku DAWA YA DENI ni KULIPA tu.
Jengine KUBWA zaidi ni kutokua na SIRI nyiiiingi. Mambo ambayo yatakufanya uwe unaweka vitu vingi ndani, ambavyo hauwezi kusema labda kwasababu ya aibu au pengine hauko huru kuviongea nalo ni TATIZO. Ni kweli sote tuna SIRI zetu, ila zikizidi ndo zinaleta msongo wa mawazo. So kuwa muangalifu na kipi unasema na kipi unaweka. Kujijazia mavitu moyoni ki afya si mpango hata kidogo.
Kalito yuko HURU, anaskiliza watu na kujifunza kila siku pia kama mimi na wewe tu, pia ana shida zake ambazo kwa kiasi kikubwa ameweza kuzifanya zisiwe chanzo cha yeye kutokua na furaha au kumpa unyonge. Pengine unaweza kusema ni kwa sababu ana hela au biashara inayomuingizia kipato kila siku ndo maana ni rahisi kwake kucheka kwa yote, ila Amini nikikuambia hata yeye huwa ana kutana na mitihani mikubwa tu, lakini kwasababu yuko POSITIVE muda wote unakuta anamalizana na shida zake kwa roho safi tu. Anakubali pale anapokua kashindwa na kujifunza na anafurahia pia challenges ambazo binafsi anazishinda kwa uzuri tu. Yeye pia ni rafiki nambari MOJA wa wafanyakazi wake karibia WOTE wa Samaki Samaki na sasa Kuku Kuku wa kuwajua mmoja mmoja kwa majina yao. Mpaka mafundi wake wote hao ni familia yake.
Wangu tumekuletea Kalito kwenye meza ili uone mambo kwa utofauti haswa. Ujifunze kutoka kwa watu ambao unawaangalia kila siku na ambao pengine unadhani mambo yao ni SUKARI kila siku iendayo kwa Mungu. Yangu matumaini utaokota mawili matatu humu. Maana ukiachana na biashara pia alizungumza maisha yake. Alivyoumwa, watoto wake na jinsi alivyofika Tanzania na nchi yetu hii na watu wake. Alituambia pia kuhusu mapenzi yake na Bahari na mahusiano yake na watoto wake na Mama yao ambaye hayuko nae tena sasa. Tafadhali enjoy.
Love,
Salama.
Soundtrack Yeah by @MarcoChali • Marco Chali Feat One T...
Follow:
Twitter: / yahstonetown
Instagram: / yahstonetown
Facebook: / yahstonetown