Salama Na SAMATTA SE6 EP49 | HEADMASTER PART 1 | SendTip MPESA LIPA NO 5578460

  Рет қаралды 133,400

YahStoneTown

YahStoneTown

Жыл бұрын

#SalamaNa #SendTip Through MPESA #5578460
Kila kijana wa ki Tanzania ambae anaupenda na kuuthamini mpira wa miguu na ambaye angependa ndo iwe kazi ya maisha yake basi Mbwana Ally Samatta ndiye role model wake, hakuna doubt kwamba watakua na mapenzi na Cristiano Ronaldo au Leo Messi au Kylian Mbappe au Marcus Rashford ila yule ambaye amewaaminisha kwamba INAWEZEKANA ukacheza POPOTE hapa duniani na hasa kwenye ligi yetu pendwa ya Uingereza ni Samatta. Rafiki tu kutoka Mbagala rangi tatu ambaye kashacheza saaana ndondo na makombe ya mbuzi wakati anakua na mwisho wa siku akaenda kucheza kwa wazungu na bado anaendelea kutafuta rizki yake huko, hata kama sio ligi ile ambayo hata yeye mwenyewe angependa awepo ila BADO ni MWAMBA wetu. Samatta huyu huyu ndo ambaye alijitwika mpira kichwani na kuitika nyavuni mbele ya beki ambae anaaminika kuwa BORA kwa misimu hii miwili mitatu ndani ya Virgil van Dijk. Hata wakati naandika hii bado mwili unanisisimka kwa wazo tu kwamba nililishuhudia lile, pata picha kwa mtoto ambaye ana ndoto hizo. Lile goli lilimfanyia NINI kwenye ndoto zake. KRC Genk walipoteza mchezo ule wa ugenini wa kombe la mabingwa wa Ulaya kwa magoli 2-1 ila kwenye mitaa yote ya mikoa ya Tanzania ile mechi ilikua ya USHINDI.
Mbwana ametokea kwenye familia ya kawaida sana sana, wazazi wake wote kama kumbukumbu yangu itakua 100 basi walikua polisi, najua kwa hakika Baba yake alikua Polisi kwa asilimia 100. Kwa marehemu Bi Mkubwa wake ndo sina hakika sana ila kwa hakika jibu limo kwenye haya maongezi yetu. Anakumbuka jinsi ambavyo Mzee wake alikua anasisitiza kwenye suala la elimu na heshima, kama mtoto wa mwisho kwenye familia hiyo, Mbwana aliupenda sana mpira, zile za kujiiba na kwenda kucheza mechi za mbali alishafanya sana na matunda ndo haya ya leo. Nadhani ilifika kipindi Mzee mwenyewe aliona basi sawa, twende huko utakako. Familia yao yote ni wapenzi wa mpira na Kaka yake Mouhamed bado anacheza hapa hapa Tanzania. Sasa akiwa kama kioo kikubwa sana kwenye jamii hii Samatta anazungumzia presha ambayo hupewa hasa pale anapoitwa kwenye timu ya Taifa, jinsi maneno mengi ya kashfa yanaporushwa kwake kutoka kwa wananchi na anakumbuka pia wakati bado anacheza T.P Mazembe kuna kipindi kocha aliacha kumuita yeye na Rafiki yake Thomas Ulimwenguna ilisemekana kama pengine hakuna na interest na team au hakua anatoa 100. Pengine kipindi hicho aliumia zaidi maana hiyo haikua jambo zuri kwake.
Mbwana anazungumza na mimi kuhusu urafiki wake na Ulimwengu na maisha ambayo walikua wanaishi pamoja wakati wako DRC, anakumbuka jinsi walivyokua wanapanga kufanikiwa pamoja na mipango yao endelevu kwenye career yao. Ulimwengu nae ana siku yake kwenye kiti chetu In Shaa Allah maana nae ana mengi ya kutuelezea. Majeraha ya mara kwa mara bila ya shaka yalisababisha kwa kiasi kikubwa ndoto zake za kucheza Ulaya kutochukua hatua ya juu kama ambavyo angependa, ila mimi naamini hayo yote maisha tu, kila kitu kilikua tayari kimesha andikwa.
Samatta ni Baba ambaye watoto wake wanasoma hapa hapa nyumbani, nilimuuliza kama watoto wake wanajua yeye ni nani na akanipa story ndogo ya yeye kung’amua kama wanafahamu fika Baba yao ni nani.
Mwenzangu humu kuna mengi sana ambayo yatakufaa na kwa nafasi ya kipekee ningependa kumshukuru Captain wa Taifa kwa kuchukua time kwenye ratiba yake ambayo ilikua imebana kweli kweli ili tu aje kutubarikia meza yetu kwa uwepo wake.
Yangu matumaini uta enjoy sana.
Love,
Salama.
Support us through anchor.fm/yahstonetown/support
SUBSRIBE TO OUR CHANNEL bit.ly/YahStoneTownSubs
Listen our Podcast on
Spotify Link spoti.fi/2Uxr6Cm‬
‪ApplePodcast Link apple.co/2Ou1bru‬
GooglePodcast Link bit.ly/GooglePodcastSalamaNa
Audiomack Link bit.ly/YahStoneTownAudioMack
‪KZbin Link bit.ly/KZbinSalamaNa
Soundtrack Yeah by @MarcoChali • Marco Chali Feat One T...
Follow:
Twitter: / yahstonetown
Instagram: / yahstonetown
Facebook: / yahstonetown
Channel Administered by Slide Digital
Instagram: slidedigitaltz

Пікірлер: 134
@mbwanamtessa8607
@mbwanamtessa8607 Жыл бұрын
Kama bado unamkubali huyu jamaa gonga like twenzetu
@Jibambeshow254k
@Jibambeshow254k 6 ай бұрын
Santa very humble and peaceful guy naona ananyayo kama za Ali hana mbwembwe and that's why he's unique ❤hii sampuli ndio kio cha jamii
@samniza1763
@samniza1763 Жыл бұрын
The first ever sensible young Tanzanian born and raised in Tanzania. Proud of who you have become.
@JJ-sx7ne
@JJ-sx7ne Жыл бұрын
Labda wewe kingereza hakipo kabisa! 98% kaongea kiswahili..
@chiconinde8135
@chiconinde8135 Жыл бұрын
Baada ile ya Jakaya....Hii tena umefanya kubwa Salama🙌⚽️💪
@rashidchimwenda
@rashidchimwenda Жыл бұрын
Big up kwa Salama kuweza kutuletea Samatta. Anaongea mambo mengi mazuri ya mfano kwa vijana wetu kwa soka letu. Ila suala la maadili sikubaliani naye aliposema ni yeye mwenyewe. Bila shaka maadili yake mazuri yamejengwa ktk familia yao (baba na mama) na hususan kwakuwa ni familia ya kipolisi, timu alizopitia hapa bongo na tamaduni zetu za kitanzania. Sisi watanzania tupo vizuri kimaadili kuliko baadhi ya watu wa mataifa mengi. Kila la heri kwake na Salama.
@arafajabir3194
@arafajabir3194 Жыл бұрын
Mungu amempa uwezo ila hapendi show off anaishi kama Ali kiba good bless you
@nellymatalanga5033
@nellymatalanga5033 Жыл бұрын
You are ths two people wamebarikiwa but wako humble na down to earth
@mzirairebeca9996
@mzirairebeca9996 Жыл бұрын
Nature ya kazi yake pia
@mzirairebeca9996
@mzirairebeca9996 Жыл бұрын
Ukiwa msanii makelele hayakwepeki
@silvanusremmy9575
@silvanusremmy9575 Жыл бұрын
Sasa Alikiba ametokea wapi. Acha makasiliko 😀
@stevewanga957
@stevewanga957 Жыл бұрын
Hes very humble like Ali Kiba...much love from🇶🇦🇶🇦
@mnasicafe1319
@mnasicafe1319 Жыл бұрын
Yeah
@GodfreyPaul
@GodfreyPaul Жыл бұрын
Much appreciation for your popa🔥🔥🔥
@sawaabyahya584
@sawaabyahya584 Жыл бұрын
Huyu mwanamme mbona best baba! Ni kioo cha jamii..... Vijana wajifunze kupitia tabia yake.... Ahsante Salama kumtafuta...
@hanssenbensonmturi2435
@hanssenbensonmturi2435 Жыл бұрын
Ulivofanya interview na Idris, nilitamani ufanye na Samatta as well. Nilivyoona hii leo, ilinikosha sana kwani Samatta ni nguli na role model to a lot of us young footballers. I am currently playing my football in The Thailand 3rd division and I dream one day not only to replicate the legend’s work but also I dream of being part of this show. Thank you Salama and Samatta for this wonderful interview
@Chemba67
@Chemba67 Жыл бұрын
Keep it up Hanssen Benson.......your name sound Danish.......
@allahisone6386
@allahisone6386 Жыл бұрын
@Hanssen God bless you ❤️🙏❤️
@shwaibukhatibu2838
@shwaibukhatibu2838 Жыл бұрын
SAMATA NA KING KIBA ALLAH BLESS YOU OTHER CELEBRITIES THEY HAVE TO COPE FROM YOU
@tatutumbi4640
@tatutumbi4640 Жыл бұрын
Salama Hongera Sana. Nafatilia Sana Vipindi Vyako. Navipenda. 👍
@albogastmselejr4583
@albogastmselejr4583 Жыл бұрын
Aiseh! Jamaa Mbona Haongei Kingereza Kama Mimi Wakati Mimi Nimekaa Week Tu Nime Sahau Kiswahili 😁😁
@jackbujimu3220
@jackbujimu3220 Жыл бұрын
🤣🤣🤣🤣 mie nimesoma tu English medium primary Ila mpka Sasa ninachanganya ngeli Kama nimeish mambele
@mussachabonga9595
@mussachabonga9595 Жыл бұрын
Fantastic interview big up sister Salama 2023
@com5766
@com5766 Жыл бұрын
The best interview Hey kenyans give likes for it
@majomamajoma8776
@majomamajoma8776 Жыл бұрын
Nina mwanangu anakupenda na anacheza mpila hatari Huwa anajiita samata, sapoti wanetu vijijin kaka nao watimize ndoto zao Allah akufanyie wepesi uzidi kung'ara
@homan_nkwama
@homan_nkwama Жыл бұрын
kama baadhi ya majibu yanatakiwa Sana ili kutimiza mahojiano ni sawa ila kama sivyo, naomba salama punguza kujenga MASWALI yanayo mlazimu mtu ajibu katika mtazamo fulani.....awe huru tusitarajie atajibu nini I LOVE YOU SALAMA
@peterkichochi7510
@peterkichochi7510 Жыл бұрын
This Guy is very humble and smart, he knows how to communicate
@ahmedjaffari9375
@ahmedjaffari9375 Жыл бұрын
Exactly… he is truly a professional footballer, may Almighty Allah bless him abundantly 🙏🏿
@maishakisunzu391
@maishakisunzu391 Жыл бұрын
Kama umegundua lafudhi ya samatta ishabadilika automatically kuwa ya kiingereza gonga like hapa😝
@navigatorelias9794
@navigatorelias9794 5 ай бұрын
Wewe acha zako babu, Asa si lazima hiyo hata wwe ukitoka kwenu huko dongo kusimamia ukija mjini lazima kiswahili chako kibadilike, so sielewi unataka kumaanisha nn
@RehemaChap3
@RehemaChap3 5 ай бұрын
Samanta MUNGU akubariki sana una busara sana
@luciasteven3314
@luciasteven3314 6 ай бұрын
Nimechelewa sn kumjua samatta❤
@erickchitumbi1308
@erickchitumbi1308 Жыл бұрын
Mbwana unayo hekima na busara sana.safi sana.
@deospackle2158
@deospackle2158 Жыл бұрын
Samatta anasound humble sana🔥🔥🔥
@nomamatata754
@nomamatata754 Жыл бұрын
I keep saying salama you got best questions for your guests.....you keep asking my questions every time i get time to see your sessions.....be blessed girl
@januarysungura8119
@januarysungura8119 Жыл бұрын
Your the best not just of luck but you deserve it keep up samatta
@ayubuakko9495
@ayubuakko9495 Жыл бұрын
Salama jabir Ur on 🔥🔥
@rosemofuga8101
@rosemofuga8101 Жыл бұрын
Waoooooo fantastic mr Samatta
@robinhomesuza8906
@robinhomesuza8906 Жыл бұрын
Naskia sauti ya ommy dimpoz zinafanana
@mountaincoffee7
@mountaincoffee7 Жыл бұрын
Noma sana
@bish_daddiyao
@bish_daddiyao Жыл бұрын
Mimi mkenya Ila Huyu Jamaa namkubali🙌🏾⚽♥️⚽
@ramadhanmaisa788
@ramadhanmaisa788 Жыл бұрын
Hakun ulazim wa kusema ww n mkenya
@mofungoya9729
@mofungoya9729 Жыл бұрын
Best player ever ♥️🇹🇿
@nadildylan6124
@nadildylan6124 Жыл бұрын
Salama tunaomba ufanye interview na nadir haruob canavaro
@jojigeorige1056
@jojigeorige1056 Жыл бұрын
He's well programmed aisee
@andrewjulius2306
@andrewjulius2306 Жыл бұрын
Sam ✊🔨 keep it up bro unjua
@safiyatheonlything7848
@safiyatheonlything7848 Жыл бұрын
leo salama na samata
@mweusiasili8345
@mweusiasili8345 Жыл бұрын
Capten Diego
@Revo_silayo
@Revo_silayo Жыл бұрын
Hyo ni nature ya intruvant peoples Huwa wanakuwa na rafiki wachche lkn wanapendwa na wengi na Huwa wanajifanyia maamuzi wenyewe na pia wapo focused na hutoboaa sanaaa.
@marwajuma7493
@marwajuma7493 Жыл бұрын
Nilisubili Sanaa asante sanaa
@user-xu2vg2ge2q
@user-xu2vg2ge2q Жыл бұрын
Uyu yomuli Dar Es Salaam Tz 🇹🇿🇹🇿🇹🇿🇹🇿
@SaidiHassan-pq3zf
@SaidiHassan-pq3zf 4 ай бұрын
Bless captain Diego
@moganfred6473
@moganfred6473 Жыл бұрын
Nakkubali sana
@googleus4903
@googleus4903 Жыл бұрын
MWAKINYO ANGEPATA NIDHAMU NA HESHIMA KAMA YA NDUGU NYETU SAMATTA ANGEFIKA ZAIDI YA ALIPO LEO.
@tztanzania2262
@tztanzania2262 Жыл бұрын
Mbona na mwakinyo yupo fresh tu!
@barbarasara4033
@barbarasara4033 Жыл бұрын
@@tztanzania2262 dharau nyingi
@mickidadybakari9974
@mickidadybakari9974 Жыл бұрын
Mwakinyo mtu poa saaana kama utam chukulia poa ila kama ukiwa mduanzi utam hulia mbona ila ni mshikaji saaana tena zaid ya saaana
@ibraimoissiaca6058
@ibraimoissiaca6058 Жыл бұрын
Popa
@dseven7094
@dseven7094 Жыл бұрын
mbagala boy
@nadildylan6124
@nadildylan6124 Жыл бұрын
Huna Baya bro
@nadildylan6124
@nadildylan6124 Жыл бұрын
Legend Bro
@daggerslick
@daggerslick Жыл бұрын
Woyoooo mbwana samatta😜😜😜
@aishaomarry6996
@aishaomarry6996 Жыл бұрын
Huyu ni mimi kabisa hua naamua mwenyewe mambo yangu.
@tztanzania2262
@tztanzania2262 Жыл бұрын
Usifanye hivyo mara zote jtahd baadhi ya mambo kuomba ushaur
@thefeyotz
@thefeyotz Жыл бұрын
Aliifunga Liverpool 😁😁
@dullayomwinyi3359
@dullayomwinyi3359 6 ай бұрын
Mwamba huyu ni hatari sana
@furahambwembwe6935
@furahambwembwe6935 Жыл бұрын
Humble man...
@xnobmedia1
@xnobmedia1 Жыл бұрын
Dah Salama kwa kumleta salama umenitouch saaaana yan. Hebu pokea 10k la soda hapooo.
@mrlabay9871
@mrlabay9871 Жыл бұрын
🔥🔥🔥🔥
@mr.graphics3213
@mr.graphics3213 Жыл бұрын
Tz oneeee🔥🔥🔥🔥
@dmikepresenter
@dmikepresenter Жыл бұрын
Samatta Goal 🇹🇿🇹🇿🇹🇿
@hansigajijime4108
@hansigajijime4108 Жыл бұрын
Mwamba kabsa
@dreamfootballclip1096
@dreamfootballclip1096 Жыл бұрын
Home boi
@flavianchuwa4370
@flavianchuwa4370 Жыл бұрын
Waaaaoooh Asante kwa hii Salama
@mwasagamwambuli3513
@mwasagamwambuli3513 Жыл бұрын
Mbwana you are what your father and mother groomed you to be what you are. Be appreciative of your parents
@mashamassingisa8738
@mashamassingisa8738 Жыл бұрын
True
@FranklinMtei
@FranklinMtei Жыл бұрын
Was looking for this. Kajikuza mwenyewe? Heshima kwa wazazi
@abuujuhayfa4321
@abuujuhayfa4321 Жыл бұрын
SAMATTA 🔥🔥🔥 gonga like kwa mwamba
@brunofernandez6608
@brunofernandez6608 Жыл бұрын
Samagoal Mbagala Boy
@hassanikipusa8328
@hassanikipusa8328 Жыл бұрын
Champion Boy 🇹🇿
@edwardfaraji1133
@edwardfaraji1133 Жыл бұрын
Sama goal Sama Sama goal....
@MariamHamad-lr3xc
@MariamHamad-lr3xc 6 ай бұрын
Kipendacho moyo dawa
@donnietommie8444
@donnietommie8444 Жыл бұрын
#SalamaNaDrLeaky
@anumario7footballlife936
@anumario7footballlife936 Жыл бұрын
Kaka yangu
@FireHouse123
@FireHouse123 Жыл бұрын
Samatta mkali sana namkubali
@kabirigisaidi8253
@kabirigisaidi8253 Жыл бұрын
Sama goal Sama goal. You de best bro
@pheninhojr5875
@pheninhojr5875 Жыл бұрын
Samagoal #hainakufel
@jamaalsaleem2926
@jamaalsaleem2926 Жыл бұрын
WA kwanza leoooooo
@samludo5435
@samludo5435 Жыл бұрын
Mlete mandonga salama
@henrymassawe699
@henrymassawe699 Жыл бұрын
😁🤣🤣🤣🤣😁😁😁😁 hatavuruga interview aiseee!!!🤣🤣
@saumusalimuhassan2499
@saumusalimuhassan2499 Жыл бұрын
Laana ya wazazi ndio hiyo mitihani.
@nahyialetomia9284
@nahyialetomia9284 Жыл бұрын
Nafurahia wewe kujenga msikiti
@MariamHamad-lr3xc
@MariamHamad-lr3xc 6 ай бұрын
Wanasema pesa ni sabuni ya roho
@mdalamgir-gu9hu
@mdalamgir-gu9hu Жыл бұрын
Yan pia salama leo ujui umulize nn..
@kanyika14kanyika16
@kanyika14kanyika16 Жыл бұрын
SAMATTA anatabia kama zangu😁😁
@kulwamwakagali24
@kulwamwakagali24 Жыл бұрын
Champs Boy
@gasorekassim5499
@gasorekassim5499 Жыл бұрын
Kizaz san
@rehemambilinyi9452
@rehemambilinyi9452 Жыл бұрын
Tuletee na pastor Tony kapola,
@cvanoedward3093
@cvanoedward3093 Жыл бұрын
Salama mbona watukatisha?
@albertbayona8441
@albertbayona8441 Жыл бұрын
Kwan jaman ilo neno shock mbona watu ulitumia vibaya
@Oldskulgemini9991
@Oldskulgemini9991 Жыл бұрын
SEMA hata wazungu hutumia Hilo neno mara nyingi Sana so Wala sio ajabu SEMA labda kwakuwa umeona wabongo pekee😅
@ahz6907
@ahz6907 Жыл бұрын
Linatakiwa litumikaje?
@kamanziian1073
@kamanziian1073 Жыл бұрын
Wewe ndo hulielewi
@kostasagelidis5326
@kostasagelidis5326 4 ай бұрын
ωχχ ο σαματαςς χαχα
@abdallahmanula1627
@abdallahmanula1627 Жыл бұрын
Apo salama umenichanganya kabla amjaaanza nyuma muanze mbele mimi cjakuelewa kabisa
@walafredchikawe4113
@walafredchikawe4113 Жыл бұрын
😂😂😂😂
@Bam268
@Bam268 Жыл бұрын
Apo mnatuchanganya Birmingham ipi sasa ya gwajima au?
@eddiearts3713
@eddiearts3713 Жыл бұрын
birmingham ni mjini ndani ndio kuna club ya aston villa
@barbarasara4033
@barbarasara4033 Жыл бұрын
Nakojoa. ..... Kwa kucheka
@mdalamgir-gu9hu
@mdalamgir-gu9hu Жыл бұрын
Tatzo utembei nawala ulizi pia mitandao uoni
@denisruvugo1764
@denisruvugo1764 Жыл бұрын
Hahahahahahahahahahahahahahaha
@adamsengo1869
@adamsengo1869 Жыл бұрын
Wape points zao wazazi maana wao ndio source ya tabia yako
@mashamassingisa8738
@mashamassingisa8738 Жыл бұрын
Masikito kua cjasikia hili kutoka kwake
@adamsengo1869
@adamsengo1869 Жыл бұрын
@@mashamassingisa8738 eti ni yeye tu amejikuta yupo ivo yani kama vile alijikuza mwenyewe, naona kama vile kwa mbali ana katabia cha kujimwambafai flani hivi
@mashamassingisa8738
@mashamassingisa8738 Жыл бұрын
Masikitiko makubwa kk
@izzi198
@izzi198 Жыл бұрын
angevuta bangi na kuwa teja mngewapa point wazaz wake? Acheni kushinikiza ujinga
@mashamassingisa8738
@mashamassingisa8738 Жыл бұрын
@izzi haya kk uko vyema sana
@nadildylan6124
@nadildylan6124 Жыл бұрын
Bro umetupa funzo kubwa cc vijana, wewe nd mchezaji usie kuwa na wajivuno na nadir haruob Kwa maono yangu
@msuyatztv5201
@msuyatztv5201 Жыл бұрын
kzbin.info/www/bejne/mICmYoGId9-bh6M Ujumbe wa wafanyakazi Kwa Mama samia
@tutumarzouk9803
@tutumarzouk9803 Жыл бұрын
mbona sama goal anajifanya kama hajui kiswahil vzr, yan kama ameish eurupe since he was childhood
@mdalamgir-gu9hu
@mdalamgir-gu9hu Жыл бұрын
Kizungu gan kazumgumza apo izo actualy nyingi..
@bryanlimbi326
@bryanlimbi326 Жыл бұрын
Sasa he was childhood ndo nini ..!? , Jifunze grammar mbwa wewe
@timmahbee
@timmahbee Жыл бұрын
@@bryanlimbi326 ilikua na ulazima wa kumtukana????
@noelsanga6853
@noelsanga6853 Жыл бұрын
@@timmahbee wivuuu tu unawasumbua
@anoldjefsta177
@anoldjefsta177 Жыл бұрын
@@bryanlimbi326 na aanze kubweka saivi
@ibrahimshilinde6129
@ibrahimshilinde6129 Жыл бұрын
Kwani wewe Salam,Nani huaga anakushauri kuwakandia vijana wenye talent za mziki?
@jilalajr_official
@jilalajr_official Жыл бұрын
@samagoal77 #diego
@baritone_online_tv2565
@baritone_online_tv2565 Жыл бұрын
Noma sana
A clash of kindness and indifference #shorts
00:17
Fabiosa Best Lifehacks
Рет қаралды 133 МЛН
A little girl was shy at her first ballet lesson #shorts
00:35
Fabiosa Animated
Рет қаралды 14 МЛН
BEHIND The GRAM (MOM & DAUGHTER) Ep 1| kajala amlilia paula kuhusu Harmonize|
3:51
Feysal Daudi Films. 457k views.5hrs
Рет қаралды 15 М.
Salama Na JOTI Ep 47 | SIMPLY SPECIAL PART 1
35:15
YahStoneTown
Рет қаралды 463 М.
❗️XOTINI YOMON QURQIB KETTI 😱😱
0:18
HUSAN_SHORTS1
Рет қаралды 4,4 МЛН
A young mother couldn't calm down her baby at the lesson #shorts
0:32
Fabiosa Best Lifehacks
Рет қаралды 12 МЛН
Finger Heart - Fancy Refill (Inside Out Animation)
0:30
FASH
Рет қаралды 25 МЛН