Рет қаралды 514
Kituo cha Utafiti wa Samaki kilichoko Wilaya ya Rorya katika kijiji cha Sota, Mkoani Mara, kimejipanga kuhakikisha wanaongeza uzalishaji wa Vifaranga ya Samaki kutokana na kuwezeshwa ruzuku iliyotoka serikalini kupitia Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) na kujenga Miundombinu ya Maabara pamoja na Majengo ya Utawala.
Teknolojia ya ufugaji wa samaki kwa njia ya vizimba inayotolewa kituoni hapo, mpakasasa imeweza kusaidia kupunguza uvuvi haramu ambapo wananchi hufundishwa kuitumia na sasa wanaitumia kufuga samaki kwenye ziwa Victoria.