VIONGOZI SADC WATOA KAULI UVAMIZI WA M23 NCHINI CONGO DR

  Рет қаралды 14,799

Mwananchi Digital

Mwananchi Digital

Күн бұрын

Mkutano wa dharura wa Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC) umesema lengo la wanachama wa jumuiya hiyo ni kuona amani inarejea mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC).
Kauli hiyo imetolewa na Rais wa Zimbabwe, Dk Emmerson Mnangagwa ambaye ni Mwenyekiti wa SADC wakati wa Mkutano wa Dharura wa jumuiya hiyo ulioitishwa jijini Harare kwa lengo la kujadili mtikisiko wa amani nchini DRC.
Hali ya usalama ilianza kuyumba nchini DRC baada ya kundi la waasi wa M23 linaloongozwa na kiongozi wa makundi ya waasi, Corneille Nangaa kuanza uvamizi na kuyashikilia maeneo ya mashariki mwa DRC ikiwemo mji wa Goma.
Kwa mujibu wa Dk Mnangagwa, suala la ulinzi wa raia nchini humo siyo la hiari bali la kisheria kwa mujibu wa makubaliano yaliyosainiwa na nchi wanachama wa SADC.
“Ni kwa bahati mbaya nasema kwamba tangu mkutano wetu wa mwisho hali ya amani imetetereka nchini DRC. Mashambulizi ya M23 yamegharimu maisha ya wanajeshi wetu wanaolinda amani DRC chini ya SAMIDRC na kuwaacha wengine wakiwa wamejeruhiwa vibaya,” amesema Dk Mnangagwa.
Pia amempongeza Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuchukua hatua za haraka za kuitisha mkutano wa dharura na wakuu wa nchi na Serikali kupitia Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama ya Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC-Troika).
“SADC inaamini kwamba kusitishwa kwa mapigano ya DRC na M23 ndiyo namna pekee ya kukomesha umwagaji wa damu nchini humo. Vikosi vyetu vya SAMIDRC vimetuhakikishia kwamba viko imara na vinaendelea kulinda amani nchini humo,” amesema Dk Mnangagwa.
Awali, Katibu Mtendaji wa SADC, Elias Magosi aliiwaeleza washiriki wanajeshi wa SADC kupitia Misheni ya SAMIDRC na Kikosi cha Ulinzi wa Amani cha Umoja wa Mataifa (Monusco) wamekuwepo nchini DRC tangu mwaka 2013.
“SADC imekuwa ni miongoni mwa jumuiya zinazohimiza na kuimarisha usalama wa DRC, vikosi vyetu vimekuwa vikitekeleza majukumu yake kwa kuzingatia sheria na miongozo ya SADC kwa lengo la kupata maendeleo endelevu,” amesema Magosi.
Amesema uvamizi wa M23 mashariki wa DRC umesababisha vifo vya walinda amani wa SADC na Monusco zaidi ya 16 huku wengine (idadi haijatajwa) wakijeruhiwa vibaya.
“Tunatoa pole kwa familia ambazo zilipotwza wapendwa wao katika mapigano ya M23 nchini DRC dhidi ya vikosi vya Serikali,” amesema.
Mkutano huo wa siku moja umehudhuriwa na viongozi mbalimbali wa mataifa ya kusini mwa Afrika akiwemo Rais Samia Suluhu Hassan (Tanzania), Dk Emmerson Mnangagwa (Zimbabwe), Andry Rajoelina (Madagascar) na Cyril Ramaphosa (Afrika Kusini), Duma Boko (Botswana) na Daniel Chapo (Msumbiji).
Marais wengine walioshiriki kwa njia ya mtandao ni Rais Felix Tshisekedi (DRC), Hakainde Hichielema (Zambia). Pia kuna Sam Matekane (Waziri Mkuu wa Lesotho), Thulisile Dladla (Naibu Waziri Mkuu Eswatini), Balozi Tete Antonio (Waziri Mambo ya Nje Angola) na wengine.
Mwisho.
VIDEO NA AMMARI MASIMBA

Пікірлер
@mapendoumoja800
@mapendoumoja800 6 күн бұрын
Wakongomani waliambiwa ikiwa MONUSCO wangaliko kwa ardhi ya congo🇨🇩 damu zitaendelea kumwagika😢 hao wakiondoka vita vitakoma😢😢😢
@selemanimmeswa3556
@selemanimmeswa3556 6 күн бұрын
Awana nguvu sadec nikama ;bure nikama umoja wa Africa
@FurahaMasudi-g3c
@FurahaMasudi-g3c 6 күн бұрын
Distraction ya viongazi wanaponda mida namuasi iko nasonga mbele mutasikiya Bukavu inaanguka
@SamsonMajula-u8f
@SamsonMajula-u8f 7 күн бұрын
Tambua kua, Congo ni baba mwenye milki nyingi amezaa watoto , baadhi ya hao watoto wapo wanao msikiliza na wengine hawataki kuendeshwa katika msingi ya baba , wakasema baba sikubali msimamo Yako na namna unavotuendesha hapa nyumbani , mtoto akaamua kujitenga na baba akaenda nchi za mbali , huko alipata marafiki na marafiki wakamuuliza ww wa kutoka wp akajieleza vizuri nimetoka kwa baba , baba angu ni tajiri lkn misimamo yake nimeikataa , marafiki wakasema sisi tunaweza kukuhifadhi lkn katutembeze tukajionee miliki ya baba ako , sisi hatuna Mali kama izo , ndipo mtoto akaamua kuungana na marafiki zake hawakutaka kuja kuongea na baba juu ya kupata haki zake stahiki kama mtoto maana anajua asingepewa kwa ukaidi aloufanya wa kukataa kuishi katika misingi ya baba ake alomzaa , wakaamua kuingia porini na kuunda kundi kubwa wamnyang'anye baba sehemu ya miliki yake kwa nguvu huku wakishirikiana na marafiki kutoka nchi za mbali na marafiki hao wanaomuunga mkono mtoto aliyekaidi madaraka ya baba wanazidi kuongezeka kila siku kwa sababu wananufaika mno na uyu baba Congo mwenye watoto wajinga sana , uku wakimuaidi kumlinda na kumuongezea nguvu ili atakaekuja ashindwe , majirani wemekua wakifanya Ivo kumlinda baba Congo juu ya vitendo vya kisaliti visivyo vya kiungwana kwa mwanae kutaka kujichukulia maeneo ambayo baba ake anatumia kumlisha lkn wamekua wakishindwa, suluhisho Anatakiwa baba akae na mwanae meza Moja, aite wajomba , mashangazi , baba mdogo , kaka na dada zake wa damu wamuulize nn hasa kijana anataka baba angali Yuko hai ampe na baba amkanye mtoto kiendeleza urafiki na hao wanaojiita watu wake wa karibu angali anasababisha uokosefu wa utulivu nyumbani kwa baba ake. 🤏
@Josephabela308
@Josephabela308 6 күн бұрын
M23 ni njia ao kilalo yaku pora mali za Congo kwa ajili ya wazungu.
@KasongoFelix-d7w
@KasongoFelix-d7w 6 күн бұрын
Wehu!! Sıo ya mala ya kwanza wanaenda kongo kurıko kumushaurı mwenzenu aende kwenye mazungumzo mnaenderea kuchochea moto , vıvyo ndıvyo mzungu anataka mmarızane!!!
@StephenMpallange
@StephenMpallange 7 күн бұрын
Amani DRC inavurugwa na kuvunjwa na Rais Tshiseked mwenyewe kwa kuwa ameshindwa kutii makubaliano ya Kenya chini ya Uenyeikiti wa Rais Uhuru Kenyata.Kuna makubaliano waliosaini kati ya Serikali ya DRC na M23,kwa nini Tshisekedi amekiuka?
@BritonNdishi-g6o
@BritonNdishi-g6o 7 күн бұрын
Apigwe kagame
@simbachui2281
@simbachui2281 7 күн бұрын
Kwa nini Yueri MSEVENI Hajasema Chochote Jamani??????????
@KasongoFelix-d7w
@KasongoFelix-d7w 6 күн бұрын
Huyo mwanamke mtanzanıa mwehu hana hakırı tımamu adanganwa na wenye msimamo mkari wa ukabıra , anaenderea kuuısha wananchı wa ke kwa kuenderea kutuma wanajeshı watanzanıa huko kongo!!!! Mtamarızıka nyi enderea mtayapata
@MelchiadeNiyuhire
@MelchiadeNiyuhire 7 күн бұрын
Pigweni
@Zuwairilla
@Zuwairilla 7 күн бұрын
Félix asikubali ayo makubaliyano awo wa m23 ni wanyarwanda WAENDE KWAO. FÉLIX AWAONDOWE KWENYE ARDHII YA CONGO. ALAFU MAZUNGUMZO YAJE BAADAE. AWO M23 NI DARAJA LA WAZUNGU KWA KUPITIYA ILI WAPORE RASILI MALI ZA CONGO
@MelchiadeNiyuhire
@MelchiadeNiyuhire 7 күн бұрын
Wacha mupigwe
@KasongoFelix-d7w
@KasongoFelix-d7w 6 күн бұрын
Wehu!! Sıo ya mala ya kwanza wanaenda kongo kurıko kumushaurı mwenzenu aende kwenye mazungumzo mnaenderea kuchochea moto , vıvyo ndıvyo mzungu anataka mmarızane!!!
IRAN YAMJIBU TRUMP, KHAMENEI ADAI AKIENDELEZA VITISHO VITAJIBIWA
5:33
Mwananchi Digital
Рет қаралды 3,9 М.
Goma DRC: SADC wakutana huku M23 wakiendeleza mashambulizi
5:55
BBC News Swahili
Рет қаралды 49 М.
Tuna 🍣 ​⁠@patrickzeinali ​⁠@ChefRush
00:48
albert_cancook
Рет қаралды 148 МЛН
“Don’t stop the chances.”
00:44
ISSEI / いっせい
Рет қаралды 62 МЛН
EXCLUSIVE!! KIONGOZI WA M23 ATAJA SABABU KUIVAMIA CONGO, ATOA MWELEKEO
10:40
ULIPOFIKIA UWANJA WA NDEGE MSALATO
4:52
Daily News Digital
Рет қаралды 7 М.
Tuna 🍣 ​⁠@patrickzeinali ​⁠@ChefRush
00:48
albert_cancook
Рет қаралды 148 МЛН