Рет қаралды 64
Kutokana na ongezeko la matukio ya tembo kuvamia makazi ya wananchi na kuleta madhara kama vifo vya binadamu Majeruhi na kuharibu mazao mkoani Simiyu mamlaka ya usimamizi wa wanyama pori TAWA imetoa vifaa vya kufukuzia Tembo kwa vikundi vilivyopewa mafunzo hayo.
Takwimu zinaonesha kwa wilaya ya Bariadi pekee mwaka 2021 watu 3 waliuawawa na tembo, watu 3 walijeruhiwa na ekari zaidi ya 1600 ziliharibiwa
Tembo ni miongoni mwa wanyamapori hatari na waharibifu ambae amekua akisumbua zaidi mkoani Simiyu husudani katika wilaya za Meatu, Itilima Busega na Bariadi.
Mwisho.