Рет қаралды 479
Watu saba wamefariki dunia na wangine wanane wamejeruhiwa katika ajali iliyohusisha Lori lenye namba za usajili T 172 AUP tela namba T 471 ABT mali ya mfanyabiashara wa mjini Bariadi aliyefahamika kwa jina moja la Lupeja kugonga bajaji yenye namba MC 426 CFQ ambayo mliki wake hajafahamika.
Ajali hiyo imetokea leo March 27, majira ya saa moja na nusu jioni maeneo ya mtaa wa kidulya nje kidogo ya mji wa Bariadi ambapo lori hilo lilikuwa limebeba tofali likitokea Wilaya ya Maswa kuelekea katika Mradi wa ujenzi wa chuo cha Veta.
Taarifa za awali kutoka kwa Kaimu kamanda wa na jeshi la zimamoto na uokoaji mkoani Simiyu Faustine Mtitu ambazo zinaeleza kuwa chanzo cha ajali hiyo ni mwendokasi wa dereva wa Lori uliosababisha ashindwe kulimudu gari na kisha kugonga bajaji.