Рет қаралды 5,176
Watumishi wawili wa kitengo cha Ardhi katika Jiji la Dodoma wamefukuzwa katika huku watatno wakisimamishwa kutokana na kusababisha migogoro ya ardhi.
Kauli hiyo imetolewa leo jijini Dodoma na Mkurugenzi wa jiji Joseph Mafuru kwenye kikao cha kamati ya Ulinzi na watumishi wapya wa idara ya ardhi.
Kikao hicho kimeitwa na mkuu wa mkoa wa Dodoma Anthony Mtaka kwa lengo la kujadili mikakati ya jinsi ya kumaliza migogoro ambayo uimetajwa kukita mizizi na kuwa eneo lenye migogoro zaidi ya mengine nchini.
Mafuru ametaja sababu iliyopelekea miongoni mwao kuingia kwenye matatizo, ni uuzaji na viwanda na kubadili matumizi ya maeneo kwa lengo la kujipatia kipato.