Рет қаралды 1,651
Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dkt. Stergomena Lawrence Tax (Mb) tarehe 01, Julai 2024 alitembelea Ofisi ya Mkuu wa Wilaya Magu mkoani Mwanza na kufanya mazungumzo na Mkuu wa Wilaya hiyo, Mheshimiwa Joshua Nassari.
Katika ziara hiyo, Waziri wa Ulinzi Tax, alipata fursa ya kushiriki Kikao cha
Baraza la Ushauri la Wilaya (District Consultative Committee - DCC) akiwa pamoja na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya, chini ya Mwenyekiti wake, Mheshimiwa Joshua Nassari.
#wizarayaulinzi #jwtz #jkt