Рет қаралды 4,147
Naibu Waziri Mkuu Doto Biteko akigusia usambazaji wa umeme vijijini mkoani Rukwa, amesema kuwa Serikali haifurahishwi na kasi ya Mkandarasi wa miradi kwani analalamikiwa kusuasua na hivyo ameagiza kuwa ifikapo Agosti mwaka huu awe amemaliza kazi na asipotekeleza agizo hilo achukuliwe hatua za kimkataba na hii inajumusha pia wakandarasi wengine wazembe ikiwemo katika Mkoa wa Kagera.
Hayo yamesemwa leo Julai 29, 2024 Sumbawanga mkoani Rukwa wakati akiweka jiwe la msingi la utekelezaji wa mradi huo mkubwa wa usafirishaji umeme wa TAZA kutoka Tunduma hadi Nakonde mpakani mwa Tanzania na Zambia.