Рет қаралды 6,137
Aliyekuwa Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) Dk Rugemeleza Nshalla amesema, kufuatia Muswada wa Sheria ya uwekezaji iliyowasilishwa hivi karibuni bungeni ni wazi faida zinazotajwa kuwepo kwenye mkataba wa DP World ni za uongo
Tayari Serikali imewahakikishia wananchi manufaa ya mkataba wa DP World ambapo licha ya matarajio ya ongezeko la mapato kutoka Sh7 trilioni inayopatikana sasa uwekezaji utakaofanywa na Kampuni ya DP World ya Dubai utaongeza mapato kufikia Sh26 trilioni.
Juni 12 ,2023 Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Profesa Makame Mbarawa akizungumza na viongozi wa dini kuhusu kuhusu mkataba huo wa awali na DP World amesema ufanisi mdogo wa bandari ndio sababu ya Serikali kutafuta uwekezaji.
Kuhusu mabadiliko ya sheria Dk Nshalla aliutaja Muswada unaopendekeza Sheria iliyotungwa mwaka 2017 kwa madhumuni ya kulinda rasilimali za nchi katika miradi ya uboreshaji na uendelezaji wa bandari.
Sheria hizo ni ile Mamlaka ya Nchi na Umiliki wa Rasimali Asilia na Sheria ya Mapitio ya Majadiliano inayohusu Rasilimali na Maliasili za nchi Sura ya 450 zote za mwaka 2017.