HAMAS YAWAACHIA MATEKA WATATU, WACHAMBUZI WASEMA ISRAEL IMESHINDWA VITA

  Рет қаралды 7,125

Mwananchi Digital

Mwananchi Digital

Күн бұрын

Wapiganaji wa kundi la Hamas wamewaachia mateka watatu wa Israel lililokuwa linawashikilia tangu uvamizi uliofanyika Oktoba 7,2023.
Katika makubaliano kati ya pande hizo, Serikali ya Israel imewaachia wafungwa wa kipalestina 183. Wafungwa hao ni waliokuwa wakitumikia vifungo mbalimbali kwenye magereza ya Israel ikiwemo adhabu ya kifo na kifungo cha maisha jela.
Mabadilishano hayo ni ya mara ya tatu tangu pande hizo zikubaliane kusitisha mapigano na kuridhia kuwaachia mateka na wafungwa wa kila pande ambapo hadi sasa mateka 15 wa Israel wamerejeshwa kuungana na familia zao huku wapalestina zaidi ya 350 wakiachiwa huru.
Al Jazeera imeripoti kuwa miongoni mwa mateka wa Israel waliokuwa Gaza walioachiwa leo Jumamosi Februari Mosi,2025, ni Rais wa Israel mwenye asili ya Ufaransa,Ofer Kalderon na raia wa Israeli ambao wote wamekabidhiwa kwa maofisa wa Msalaba Mwekundu mjini Khan Younis.
Baada ya saa moja kupita, Hamas pia imemuachia raia wa Israel mwenye asili ya Marekani, Keith Siegel ambaye amekabidhiwa kwa maofisa wa Msalaba Mwekundu waliokuwa eneo la Kaskazini mwa Gaza nchini humo.
Muda mfupi baada ya raia hao kuwasili nchini Israel, magari yenye wafungwa 183 wa kipalestina wakiwemo watoto waliokuwa kifungoni nchini Israel katika utekelezaji wa makubaliano ya kusitisha mapigano hayo yaliyofikiwa Januari 19,2025, Doha nchini Qatar.
Wafungwa 73 kati ya 183 wa Palestina walikuwa wakitumikia adhabu ya kifungo cha maisha katika magereza mbalimbali nchini Israel.
Tayari basi la kwanza lililobeba wapalestina 32 kutoka gereza la Ofer nchini Israel limewasili mjini Ramallah ukanda wa Magharibi mwa Gaza, huku wakipolekewa na mamia ya raia waliokuwa wanawasubiria eneo hilo.
Miongoni mwa walioachiwa ni wazee wa Kipalestina waliokuwa kifungoni kwa muda mrefu nchini Israel kutokana na mzozo wa pande hizo ambao umedumu kwa karibia nusu Karne, wengine walikuwa kwenye viti vya kusukuma (Wheelchair).
Mbali na hao, wapalestina 111 kati ya 183 walioachiwa leo walichukuliwa na majeshi ya Israel baada ya shambulizi la Oktoba7, 2023. Baada ya kuachiwa, saba kati yao watapelekwa uhamishoni nchini Misri.
Inakadiriwa kuwa kuna wapalestina takriban 4,500 katika magereza ya Israel wakitumikia vifungo mbalimbali wakishikiliwa katika kile kinachoitwa ni vifungo vya kiutawala ambavyo vinawazuia kushtakiwa badala yake kuamriwa kutumia kifungo jela bila kushtakiwa.
Mapema leo asubuhi wapiganaji wa Hamas wameonekana wakipanga mistari huku wakiwatuliza umati wa raia wa Palestina waliojitokeza kushuhudia kuachiwa kwa mateka hao eneo la Mji wa Gaza na Khan Younis. Baada ya kufikishwa, mateka hao, Kalderon, Bibas na Siegel waliwapungia mikono umati huo.
Mateka wote wameshafika nchini Tel Aviv nchini Israel ambako watafanyiwa uchunguzi wa kitabibu kubaini hali ya afya zao kabla ya kuungana na familia zao.
Hadi sasa hali za kiafya za mke wa Bibas na watoto wawili waliochukuliwa mateka na Hamas bado hazijulikani zikoje.
Luciano Zaccara, ambaye ni Profesa wa Chuo Kikuu cha Qatar aaliyebobea katika mzozo ya Mashariki ya Kati anasema kuachiwa kwa mateka hao ni ishara kwamba Hamas bado ina nguvu ya kuendelea kulisimamia eneo la Gaza pamoja na mashambulizi mfululizo ya IDF yaliyofanyika eneo hilo kwa miezi zaidi ya 15.
“Pamoja na kuwa Israel ilidai kuwasambaratisha Hamas lakini picha hazidanganyi kwamba Hamas bado wapo na bado wanamsukumo kwa Umma,”
“Mabadilishano haya yanafanyika bila kikwazo chochote kiasi kwamba yanatoa picha kwamba huenda mabadilishano yanayofuata huenda yasiwe na changamoto yoyote,” amesema Profesa Zaccara.
Mchambuzi wa Siasa za Mashariki ya Kati kutoka Chuo Kikuu cha Burzeit, Basil Farraj amesema kuachiwa kwa wafungwa wa palestina hakuondoi maumivu ya wapalestina na Hamas ambayo yameyapitia kwenye mashambulizi mfululizo ya Israel katika ardhi yao.
Ametahadharisha kuwa baada ya mabadilishano hayo huenda Israel ikarejea tena kuwakamata raia hao wa Palestina na kuibua tena mzozo kati ya pande hizo.
Kulingana na makubaliano hayo, siku ya Jumanne huenda mateka zaidi ya 60 wa Israel wakaachiwa huku wafungwa wa Palestina wengi zaidi wakaachiwa kutoka katika magereza ya Israel.
Makubaliano ya kusitisha mapigano kati ya pande hizo yaliratibiwa na mataifa ya Qatar, Marekani na Misri.
Wakati mabadilishano hayo yakifanyika, Shirika la Afya Duniani (WHO) limesema wapalestina takriban 50 wako kwenye uhitaji wa hali ya juu wa kupatiwa matibabu nje ya nchi hiyo na wanatarajiwa kuvushwa kupitia mpaka wa Rafah kuhudhuria matibabu hayo.
Pia Jeshi la Israel (IDF) linashutumiwa kutekeleza shambulizi kwa kutumia boti iliyokuwa ikipita baharini na kurusha risasi karibia na Kambi ya Wakimbizi ya Nuseirat Gaza nchini humo na kusababisha kifo cha mvuvi katika eneo hilo.

Пікірлер: 43
@MfiriNasawe
@MfiriNasawe 6 күн бұрын
Hamasi bado wanaguvu ,ogopa watu wanaopigania imani usiwalinganishe na wapiganaji wa mshahara
@MasterOil-qm6vw
@MasterOil-qm6vw 6 күн бұрын
Lakin pia jeshi linapo ingia vitani linakua namalengo israel walipo ingia gaza walikua na malengo makuu 3 kwanza kuwakomboa mateka 2 kuwamaliza hamas 3 hamas isitaawale tena gaza sasa kwenye haya malengo hakuna hata lengo moja ambalo isarel ameweza sana ameuwa raia na wanawake na wazee na kupiga mashule na hospital hiyo ndio maana ya kushindwa vita
@mussammanga7791
@mussammanga7791 6 күн бұрын
Na ndio maana waphalestine wanafurahi kwasbb wameshinda vita.
@stanleyamlima2085
@stanleyamlima2085 6 күн бұрын
Kwanini wajifiche mashuleniii
@KhalidiBoaz
@KhalidiBoaz 6 күн бұрын
Hapa GAZA,HAPATAKUWA NA UTAWALA WA HAMAS,HUO NI USHINDI WA KWANZA WA ISRAEL,NGOJA TUSUBIRI MAJIBU YA MASWALI MENGINE
@saidimpako5186
@saidimpako5186 6 күн бұрын
@@stanleyamlima2085 vita ni mbinu kaka hata mpira timu ikikufunga goli moja wanapakibasi dakika 90 zinamalizika na wanashinda
@MohamedOmari-y1t
@MohamedOmari-y1t 6 күн бұрын
Mateka aliokoa wangapi?​@@KhalidiBoaz
@MasterOil-qm6vw
@MasterOil-qm6vw 6 күн бұрын
Wew uliskia lini palestina ama hamas wanataka vita visimame wakati hao mashoga wa israel ndio wanaotaka vita visimame hamas wao wanakuja na masharti yao kwamba ili tusimamishe vita lazima wazayuni waondoke kwenye maeneo ya palestina na wafungwa walioko israel waachie kinyume na hivyo ni mwendo wa chuma
@mbwanarajab7238
@mbwanarajab7238 6 күн бұрын
Aliyeapa kwamba hatazungumza na Hamas juu ya amani leo kafuata mashariki ya Hamas.....
@AsiaAsi-s3u
@AsiaAsi-s3u 3 күн бұрын
Wanaumehaooo!!
@Mzalendo-n8q
@Mzalendo-n8q 6 күн бұрын
Nadhan ukiangalia tu utajua kati ya hamas na waizraeli..nani ni watu wazuri..hamas hawashiki wananchi ovyo ovyo wala watoto lakn izrael wanashika hadi watoto wadogo kiwapeleka magerezani
@allymuhammad8956
@allymuhammad8956 6 күн бұрын
Duh hawa jamaa hatar yaani siku zote israil haijafanikiwa kuwakomboa na wamewarejesha wapo hai tena wazima wa afya hawa kiboko wa dunia
@salimabdallah5176
@salimabdallah5176 5 күн бұрын
SASA DUNIA INA PELEKA MAJESHI MAFUNZO ISRAEL 🇮🇱 AU HAMAS
@daudigabriel700
@daudigabriel700 5 күн бұрын
Wameua ndugu zetu watanzania, halafu unasema hamas watuzuli
@hassanhamza9247
@hassanhamza9247 5 күн бұрын
Ndio kifo Chao kilipopangwa apo
@Williamstozzo
@Williamstozzo 6 күн бұрын
Ulitegemea Al Jazeera waseme israel kashinda?? Hamas wamechezewa mchezoo ,, netanyahu anataka mateka watokee na apunguze maandamanoo alafuu vitaa inaanza upyaa😢
@fatumahamisi-m1e
@fatumahamisi-m1e 6 күн бұрын
Akili yako imekaa kikafiri kafiri.
@MfiriNasawe
@MfiriNasawe 6 күн бұрын
​@@fatumahamisi-m1esawa,hata akianzisha vita tena bado hatawe Hamasi sii wanajeshi wa mshahara,wangekua wa mshahara hamasi ingekuwa ishapotea zamani lakini hamasi haitakaa ipotee lambda mungu awapatanishe ugomvi uishe
@Rawdha-y8t
@Rawdha-y8t 6 күн бұрын
utadhan huyo netanyahu akikukuta atakuacha salama na ujue huko palesta wapo wakrso kibao so kama ni ukristo unakufanya uwe uoande wa wayahudi ujue myahudi hata haamini kua Yesu hupo wao wanaamin badoooo hata haja zaliwa
@IbrahimBinbenya
@IbrahimBinbenya 6 күн бұрын
Mwache afanye ndani ya wiki nyetanyanyahu ni maiti
@KhalidiBoaz
@KhalidiBoaz 6 күн бұрын
Kuna wale wanaosema,eti ISRAEL IMESHINDWA VITA,MIMI KAMA MSOMI MKUBWA NASEMA 🇮🇱 ISRAEL AMESHINDA KWASABABU ZIFUATAZO,1.HAPATAKUWAPO NA UTAWALA WA HAMAS TENA GAZA,HATA HATA KAMA WATAKUWEPO BASI UTAKUWA NI KAMA UTAWALA WA PANYA MBELE YA PAKA,2.KWA SUALA LA MATEKA,HILO HALINA MASHIKO KWANI LENGO LA HAMAS 7OCT.2023,ILIKUWA SIO KUBADILISHA MATEKA BALI NI NIKUDAI UHURU WA PALESTINE.3.VIONGOZI WOTE WA JUU HAWAPO TENA,K.M.YAHAYA SINWARI,zMOHAMED DIEFF,ISMAIL HANIYE K.N SASA NASHANGAA KUONA ETI PALESTINE AMESHINDA VITA😂😂😂😂😂
@Rawdha-y8t
@Rawdha-y8t 6 күн бұрын
watatu kwa 100 huna akili kweli mshamba mmoja wewe
@daudimaniseli759
@daudimaniseli759 6 күн бұрын
WE KIAZI MVIRINGO LINI UMESIKIA HAMASI IKA TETELEKA KIUONGOZI ,, NAFASI ZOTE ZIMEJAZWA...NYIE WAPIGANIA TUMBO MMESHINDA KILAKITU YANI ISRAEL NA MANDONGAAA IS BETTER NIMANDONGAAA
@KhalidiBoaz
@KhalidiBoaz 6 күн бұрын
@@daudimaniseli759 BISHA KWA HOJA NA SIO KUTUKANA,LETA HOJA MEZANI NAMI NITALETA ZANGU MEZANI THEN TUTAPIMA ZIPI ZENYE NGUVU
@jombadulla
@jombadulla 6 күн бұрын
ci sabab hyo,viongozi wa ngapi wa kiislm duniani wameondoka au wamwfungwa,lkn vp apo,waislm bado wanakuja na viongozi zaid ya wale,hasan nasrallh,kaja mzur kuliko yule,we vp
@AliAbdallah-i6h
@AliAbdallah-i6h 5 күн бұрын
​@@jombadullailo jamaa choko tu
@GeorgeElias-p5o
@GeorgeElias-p5o 6 күн бұрын
Imeshindwa vip vita na mnalalamika raia wa palestina wanakufa waache mapigano
@AbdallahJuma-f8y
@AbdallahJuma-f8y 6 күн бұрын
Kwani dhumuni lao lakupigana vita la Israel lilikua Nini ?
@alihaji215
@alihaji215 6 күн бұрын
Kwani vita ni kupigana na majeshi au kupiga raia na ingekuwa ni hivyo basi dunia isingekuwepo,inaonaonesha hujuwi loloye we upo tuu.
@SalumSaid-w8i
@SalumSaid-w8i 6 күн бұрын
Niaambu taifakubwa kama marekani na wazayuni kushindwa kuwa ondowa hammasi badlands yake wana waweka gerezani watoto😂😂😂😂😂 ukafiri kitu ovyo sana mtoto una mshikilia au kumuuwa kabisa kweli hilo nitaifa lamungu wakrito munao jipoga kifuwa mayahudi niwetu na mupo ktkt njia ya mungu jee hii nihaki nauliza maya hudu website unapo unga mkono uwovu nawewe umo ktk kundi mayahudi weusiwatoto wangapi wamekufa na wazee mutamjibu nn aliye waumba iki mm mumekosa jibu sahihi lakuni jibu moto una wasubiri
@Williamstozzo
@Williamstozzo 6 күн бұрын
Na maeneo yao wanaporwa Kila sikuu
@abdullahmanalex2306
@abdullahmanalex2306 6 күн бұрын
Mbumbumbu WEWE kuuwa Watu wasiojiweza WA mama na watoto sio kushinda vita ,, tambua vita ni malengo
@JohnMwashalamila
@JohnMwashalamila 6 күн бұрын
Mbona hamax hawaish jmn
@abdullahmanalex2306
@abdullahmanalex2306 6 күн бұрын
Waende wapi Watu WA Mungu😂
Hamas releases three Israeli captives
11:18
Al Jazeera English
Рет қаралды 8 М.
HAMAS IMEWAUA MATEKA NANE WA ISRAEL, NI WALIOPASWA KUACHILIWA
5:18
Mwananchi Digital
Рет қаралды 4,1 М.
Antony Blinken Says the War in Gaza Won’t Define His Legacy
50:08
New York Times Podcasts
Рет қаралды 58 М.
Israeli Soldier's Explosive Tell-All: "Palestinians are Right to Resist"
27:08