Рет қаралды 7,242
Bondia Karim Mandonga atapanda Ulingoni July 29 dhidi ya Bondia Golola Moses kutoka Uganda, Pambano litapigwa Mwanza.
Mandonga ametoa Msemo mpya 'NDUKUBEE' ndio ngumi anayokwenda kumchakaza nayo Golola hiyo Tarehe 29.
Aidha ametoa maoni yake juu ya Mpira wa Miguu na kueleza kuwa kwa sasa anakaa katikati Ya Simba na Yanga kama Mzalendo, japo Yanga ndio anaipenda zaidi.
Pia amejibu kuhusu Bondia Hassan Mwakinyo juu ya kauli zake kwa Wacheza Masumbwi na hapa Karim amekiri kuwa hamfahamu Mwakinyo kama ni Bondia.