Рет қаралды 24,692
Mbunge wa Gairo, Ahmed Shabiby amesema kuwa wapigaji wa fedha za umma wamekuwa wengi, na wamejikita kwenye kusifia kuwa 'Mama Anaupiga Mwingi,' lakini kiuhalisia wao ndio wanaoupiga mwingi kwa kuiba fedha za umma.
Amesema hayo bungeni jijini Dodoma wakati akichangia Bajeti ya Serikali na Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa mwaka 2024/25 na kuongeza kuwa utaratibu wa kuacha taasisi kukusanya fedha unachochea vitendo vya wizi wa fedha za umma.