Рет қаралды 693
Mwanza. Wavuvi wamelalamikia kurejea kwa uvuvi haramu katika ziwa Victoria hali inayotishia kupotea kwa samaki na kuiomba Serikali kushughulikia jambo hilo.
Wakiwasilisha kero zao Octoba 4, 2023 mbele ya Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega kwenye soko la Kimataifa la Kirumba lililopo jijini Mwanza kwa lengo la kusikiliza kero za wavuvi na wafanyabiashara.
Wavuvi hao wamesema sokoni kumekuwepo na ongezeko la samaki wadogo wanaovuliwa kwa kutumia nyavu ambazo haziruhusiwi kinyume chake samaki wakubwa wamepungua hali inayoibua hofu kwa vizazi vijavyo kukosa samaki.