Рет қаралды 138,715
"HOJA ZA PROFESA KISHIMBA BUNGENI"
.
.
"Kuna sheria mpya imeanzishwa ambayo inamtaka mtu atakayekuwa na gunia moja la mkaa lazima apte kibali toka Halmashauri ya Wilaya na awe na EFD, labda wenzetu wangeangalia Jiografia ya nchi na maisha ya watu wetu. Tutarajie ndani ya mwezi mmoja kutatokea "chaos" kubwa ya mkaa na kwa kawaida itawezekana kweli watu wasipike na wasile?. Kuna majimbo kutoka makao makuu ya Halmashauri kwenda kijijini ni zaidi ya kilomita 200 kweli mwananchi mwenye gunia moja aende mpaka wilayani?"
"Kwetu kanda ya Ziwa ukimwambia mtu apande miti kwa ajili ya mvua anakuona ni mpuuzi maana yake tuna mafuriko miaka miwili, mwananchi atakuuliza je unataka tupande miti ya kuzuia mvua maana ukiwaambia unataka miti ya mvua wanakuuliza kuzidi hii iliyopo leo. Sisi tuwaambie panda miti ya kutengeneza pesa"
"Wakati mwingine mnasema tunawasakama wasomi, leo Tanzania ni nchi ya nne kwa ku-export mkaa wa magendo, sasa ukataaje kurasimisha ili upate pesa na wale wanaonunua wa magendo waje kununua pale kwenye soko.”
“Haiwezekani baada ya miaka 60 tukawapeleka watoto wasome wawe mgambo wa kukamata wazazi wao, kazi ya elimu duniani ni kutatua matatizo.
"Leo wazungu wametengeneza mpaka mapapai ya miezi 6, wametengeneza kuku wa kizungu kwanini hao wataalamu wasilete miti ya miezi 6 ili watu wauze kuni na mkaa, lazima twende kwenye pesa" Jumanne Kishimba-Mbunge Kahama Mjini
#KutokaBungeni
#CloudsDigitalUpdates