Рет қаралды 27,996
Mbunge wa Kahama Mjini (CCM), Jumanne Kishimba ameitaka Serikali kufanya mabadiliko ya sheria na kanuni mbalimbali zilizorithiwa kutoka kwa mkoloni ili kumrahisishia mwananchi wa hali ya chini maisha.
Kishimba amehoji juu ya adha ya wanaodhamini kesi vijijini kuwa ni watumishi wa serikali pekee na kuwaacha wanakijiji aliowaita watu wa Ng'ombe kuwa wenyewe ndio wenye mali na wakati ambapo kwenye masuala ya kijamii kama vile ndoa Ng'ombe ndio wamekuwa wakitumika kama mahari.
"Leo ukipata kesi unatakiwa udhaminiwe na mtu ambaye ni mwaajiriwa wa Serikali, unakataaje mtu wa Ngombe kunidhamini mimi, na Ng'ombe mwenyekiti sisi ndio tunaolea mke, hauwezi kuoa kwa friji au TV, huyu mtumishi wa serikali anamiliki TV na friji" Aliongeza Kishimba
Kishimba amezungumza haya leo wakati akichangia maoni yake kwenye Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2024/2025 pamoja na Mapendekezo ya Mwongozo wa Maandalizi ya Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2024/2025 bungeni jijini Dodoma. P