RAIS DKT. MAGUFULI AWASIMAMISHA TBA KUJENGA NYUMBA ZA MAGEREZA UKONGA

  Рет қаралды 132,445

Ikulu Tanzania

Ikulu Tanzania

Күн бұрын

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli tarehe 16 Machi, 2019 amefanya ziara ya kushtukiza katika mradi wa ujenzi wa nyumba za makazi ya Askari Magereza wa gereza la Ukonga Jijini Dar es Salaam na kuagiza mradi huo ukabidhiwe kwa Jeshi la Ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ).
Mhe. Rais Magufuli ametoa maagizo hayo baada ya kubaini kuwa Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) imeshindwa kutekeleza mradi huo kwa wakati, licha ya Serikali kutoa shilingi Bilioni 10 za ujenzi.
Ametaka wataalamu wa TBA waliokuwa wakisimamia mradi huo pamoja na Askari Magereza waondoke na kuwapisha JWTZ.
“Kwa hiyo hapa nisimuone mtu wa TBA, nisimuone mtu wa Magereza kuja kusimamia, muwaache Jeshi la Wananchi wafanye kazi zao, siku watakapokuja kunikabidhi na mimi nitawakabidhi Magereza, kwa hiyo watu wa TBA kuanzia leo nimewafukuza hapa” amesema Mhe. Rais Magufuli.
Mhe. Rais Magufuli ameelezea kutoridhishwa na utendaji kazi wa TBA katika mradio huo ambao ulianza zaidi ya miaka 2 iliyopita kwa kushirikisha Jeshi la Magereza ambalo lilikuwa linaisadia TBA katika kazi za ujenzi, na ametaka TBA na Jeshi la Magereza wabadilike katika utekelezaji wa majukumu yao.
“Nataka kila mlipo watu wa Magereza mfanye kazi, msimamie watu, kama ni ng’ombe muwafuge vizuri wazalishe vizuri hadi muuze mazao nje, kama ni kilimo mlime kwelikweli, muwe ni jeshi la kuzalisha, hii ni aibu kuleta jeshi jingine la wananchi kuja kuwajengea nyumba nyinyi, wakati nyumba mnakaa nyinyi, mlitakiwa muwe mmeshapanga mkakati kwamba TBA wamesuasua, ngoja tufyatue matofari, tuanze kujenga” amesisitiza Mhe. Rais Magufuli.
Mkuu wa Utawala wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) Kanali Charles Mbuge amesema JKT itakamilisha ujenzi huo ndani ya kipindi cha miezi 2 na nusu kuanzia kesho na kwamba kazi zitafanywa usiku na mchana.
Aidha, Mhe. Rais Magufuli ameitaka TBA kutoa maelezo ya namna fedha zilizotolewa na Serikali kiasi cha shilingi Bilioni 10 zilivyotumika, na ameonya kuwa endapo itabainika matumizi ya fedha hizo hayaendani na kazi zilizofanyika hatua kali zitachukuliwa.
Katika mradi huo, ujenzi wa majengo 12 ya makazi ya Askari Magereza yaliyopangwa kuwa na ghorofa 4 kila moja ulioanza Desemba 2016 umefikia asilimia 45 tu na unaendelea kwa kusuasua.

Пікірлер: 88
@abduladhimually3542
@abduladhimually3542 5 жыл бұрын
Jembeeee#watakubalitu..........your a good leader never met before
@nyanda427
@nyanda427 5 жыл бұрын
Waoh. Love you Mr. President Dr. John Pombe Magufuli
@sk-wj9or
@sk-wj9or 5 жыл бұрын
I salute you Mr president!
@neemajoshuaer9562
@neemajoshuaer9562 5 жыл бұрын
Saf Sana mhe Rais
@freddymello3227
@freddymello3227 5 жыл бұрын
Neema Joshuaer ,mambo!!uko poa neema wng
@ramadhanimmana3829
@ramadhanimmana3829 5 жыл бұрын
Safi saan mkuu
@amos878
@amos878 5 жыл бұрын
Outstanding mkuu na waje walale na wafungwa wao 😂😂😂😂
@olembetonga7341
@olembetonga7341 3 ай бұрын
😂😂
@BonivenjaNation
@BonivenjaNation Жыл бұрын
Uko ulipo Mungu azidi kukulinda
@jacksonjombo7221
@jacksonjombo7221 9 ай бұрын
God give me a vision like this Father, Ee Mungu nipe maono kama uyu Baba
@j.bjacobbasubi2187
@j.bjacobbasubi2187 8 ай бұрын
I'm a congolaise but 😢😢😢
@amirimbago8325
@amirimbago8325 8 ай бұрын
Nikikupa maono watakuua mapema...pambanatuu na hali yako kwa maendeleo ya ukoo wenu.
@bundalamlolasa3774
@bundalamlolasa3774 5 жыл бұрын
Safe Sana mheshimia Rais Kaz yako inaonekana.
@mohdsalum3832
@mohdsalum3832 5 жыл бұрын
Safi sana
@allyfutto8763
@allyfutto8763 5 жыл бұрын
Faraja iliyoje kubahatika amirijeshi anayeona mbalisana watanzania ni jambo la kujivunia sana ni mipango ya mungu Tumeteseka sana Tubadirike twende na wakati.
@freddymello3227
@freddymello3227 5 жыл бұрын
Sifa ya kiongozi bora ni kuchukua hatua katika muda mwafaka. hongera J.P.M kwa hatua hii uliyochukua.hakika wewe ni mfano wa kuigwa kwa vizazi vijavyo. aina ya uongozi wako ni wito na kujitoa kweli kweli.nchi yetu inauozo kila sehemu. Viva C.C.M,viva J.P.M
@JoasDioniz
@JoasDioniz 5 жыл бұрын
Haaaaahaaaaa lazima wazitapike #JeshiHalishindwi #TanzaniaMpyaYaJPM
@aloycekiwia8613
@aloycekiwia8613 5 жыл бұрын
Hata Umchukie vipi Uncle Magu, Kuna mambo mengine lazima umkubali tu! labda uwe Chizi.!? Hizi nyumba nazikumbuka ni miaka mingi kweli. Kumbe walishapewa na Pesa zote.!!??
@kwandukanunda4351
@kwandukanunda4351 5 жыл бұрын
Watapike
@shabanmlekwa9513
@shabanmlekwa9513 5 жыл бұрын
Na Tanzania ndo ilishafikia hapo. Alitakiwa aje mtu ka Magufuli.
@zefamange7281
@zefamange7281 5 жыл бұрын
KMBIZA HAO COMMANDO WANGUUU, WAMEZOEA UJINGA UJINGA HAO
@neozoran244
@neozoran244 5 күн бұрын
Evaluation ya billion 10 yangu mtasema mmezitumiaje.., R.I.P Our lovely Leader
@hamisiramadhani6620
@hamisiramadhani6620 5 күн бұрын
"Jeshi halishindwi" R.I.P Mej General Mbuge 🕊💔
@victustemba
@victustemba 5 жыл бұрын
Hapa kazi tu, 10% watazitapika..!😀
@gooddeeds162
@gooddeeds162 5 жыл бұрын
Victus temba Shemeji Nafurahi sana hatua anazochukua Mh Rais zinatia sana Faraja, Lakini Kuna wachache wanataka kuzingua tu . Watashindwa tu
@masigomhoja5182
@masigomhoja5182 5 жыл бұрын
Safi sana duh kura yangu mimi ni yakoo mjombaa
@tufyambefredrick4340
@tufyambefredrick4340 5 жыл бұрын
Ukimuona mh Raisi amevaa hiyo kofia na yuko kwe ziara ujue kuna jambo litatokea nani anakubali hii
@shukurumwangosi1537
@shukurumwangosi1537 5 жыл бұрын
Wooh
@nassoromzenga866
@nassoromzenga866 5 жыл бұрын
Napenda sana mamuz ya rais anataka wachapa kaz
@magilemabula5755
@magilemabula5755 5 жыл бұрын
Tanzania kwanza
@agneomasonda2462
@agneomasonda2462 5 жыл бұрын
Piga kazi baba
@RedpilledPhoenix
@RedpilledPhoenix 5 жыл бұрын
Mungu mlinde Rais wa 🇹🇿 namwombea afya nzuri
@ismailyusuph740
@ismailyusuph740 5 жыл бұрын
....NA WATAITAPIKA...! JESHI halishindwi Mh Rais...!
@h2kizzyboymsafi832
@h2kizzyboymsafi832 5 жыл бұрын
Safi sana jembe
@mussamkali9926
@mussamkali9926 11 ай бұрын
Magu kazini
@allythabit5175
@allythabit5175 5 жыл бұрын
raha sana
@maduhansanga109
@maduhansanga109 5 жыл бұрын
Nakukubali sana rais wetu
@tanzania2559
@tanzania2559 5 жыл бұрын
🙌🏾🙌🏾🙌🏾👏🏾👏🏾👏🏾👏🏾👏🏾
@shayoyahaya3736
@shayoyahaya3736 5 жыл бұрын
Sipata ona...!! Huyu ni zaidi ya Rais. Washa moto haya ndio mabadiliko ... Walishazoea ubwenyenye....
@zawadix9574
@zawadix9574 5 жыл бұрын
Jembe
@mupagedragon1972
@mupagedragon1972 4 жыл бұрын
Vizur sana baba etu magu
@godfreymwacha8711
@godfreymwacha8711 5 жыл бұрын
That my president I salute you
@kahmardintebe9266
@kahmardintebe9266 11 ай бұрын
Chuma hakika mungu alituzawadia Ila hatukuona umuhimu wake pumzika kwa amani jpm
@gabrieladam491
@gabrieladam491 5 жыл бұрын
Huwa nakuelewaga Sana naomba Mungu anipe nifanye kama wewe President
@pacomezouzoua9175
@pacomezouzoua9175 3 ай бұрын
Chuma kweli kweli daah Why God ulimchukua mapema 😢
@AbdilahiMohamed-l1y
@AbdilahiMohamed-l1y Ай бұрын
Walimuuwa
@goodlegacytv5068
@goodlegacytv5068 3 ай бұрын
Duh mwamba kabisa
@VictorSakawa-e2s
@VictorSakawa-e2s 6 күн бұрын
Kiongozi shupavu😊
@utukufueliya5279
@utukufueliya5279 5 жыл бұрын
kwa kauli hii kuna watu wanaenda kufungwa.....
@Lusekelo98
@Lusekelo98 4 ай бұрын
Real life
@benbranco3688
@benbranco3688 3 жыл бұрын
R.I.P MKUU DAHH
@saeedelbahsany2102
@saeedelbahsany2102 Күн бұрын
Rest in peace Mbuge
@athumanomary1438
@athumanomary1438 5 жыл бұрын
Ewe mwenyez MUNGU ewe mwenyez MUNGU tunakuomba na tunazidi kukuomba enderea kumuongoz kumsimamia kumrinda na kuzidi kuimarisha afya yake raisi wetu ewe mwenyez MUNGU mkuu
@barakamashinga463
@barakamashinga463 5 жыл бұрын
A cleansheet president!
@samsonmagesa3959
@samsonmagesa3959 5 жыл бұрын
Hapo ndipo waga Nasema 2020 Kura yangu Kwakoooooo
@samsonmagesa3959
@samsonmagesa3959 5 жыл бұрын
Jeshi halishindwi huko Vizuri Kanali
@vincentmasanja789
@vincentmasanja789 5 жыл бұрын
Inawezekana Raisi wa awamu hii akaweka historia ya pekee ,kwa kuwa nchini bila kwenda ughaibuni kwa miaka minne.
@fathermore9772
@fathermore9772 5 жыл бұрын
Vincent Masanja tuseme asante kwakua nakiongozi mwenye mtizamo chanya namsimamo kama uncle
@vincentmasanja789
@vincentmasanja789 5 жыл бұрын
Hakika Fadher More.
@raphaelkessy7360
@raphaelkessy7360 7 ай бұрын
Pumzika kwa amani na baraka Kamanda mkuu JPM
@kolinsimahanga9845
@kolinsimahanga9845 5 жыл бұрын
jwtz safi
@ulemse6067
@ulemse6067 5 жыл бұрын
Twahitaji kiongozi Kama huyu huku Kenya.
@manyotaskipper5765
@manyotaskipper5765 5 жыл бұрын
Ukinuna UWE NA SABABU MJOMBA MAGU BADO WANAJUSAHAU TBA WANALALA TU
@tevintevin1884
@tevintevin1884 5 жыл бұрын
Hadi raha ...bravo Mr President... Hao wa kuzitapika itabidi watapike mpaka nyongo
@jamessanga2176
@jamessanga2176 5 жыл бұрын
hahahahahah
@matingo-bk1248
@matingo-bk1248 5 жыл бұрын
Hii ndio maana halisi kiongozi, kuwa na maamuzi magumu mambo yanapoenda sivyo
@utukufueliya5279
@utukufueliya5279 5 жыл бұрын
Kazi usiku na mchana.... 😀😀😀😀😀😀
@florencebudoya3814
@florencebudoya3814 5 жыл бұрын
Elelo yeye.
@lengaiolesabaya8209
@lengaiolesabaya8209 5 жыл бұрын
Mungu unatisha.Unajua kuwaleta watu wako kwa saa zako, kuliponya taifa lako.
@samuelmwaikambo5691
@samuelmwaikambo5691 5 жыл бұрын
President JPM nadhani bado hawajakuelewa hao wanafanya wajuavyo ni pingu tu huko ni kuhujumu mali ya watanzania walipa kodi usiku na mchana.
@abdilahijuma2852
@abdilahijuma2852 5 жыл бұрын
Dr magufuli safi sana
@PetroKimola-k2k
@PetroKimola-k2k 19 күн бұрын
M😅😅😅 miaka na usheee
@ismailmasoud6001
@ismailmasoud6001 4 ай бұрын
Aisee huyu jamaa alikua ni MWAMBA kabisa..!
@thomasmollel9465
@thomasmollel9465 7 ай бұрын
Rest in peace kipenzi cha watanzania
@joesimba
@joesimba 2 жыл бұрын
2:50
@EmmanuelNicolas-n9l
@EmmanuelNicolas-n9l 9 ай бұрын
Jaman ludi kigambon uvukaji feery tunateseka panton kla sku zinaalibika tunateseka
@SaleheMkomwa
@SaleheMkomwa 4 ай бұрын
Fukuza tu
@mickwealthy500
@mickwealthy500 Жыл бұрын
RIP
@PatelMpene
@PatelMpene 7 ай бұрын
Hahahaha et ntawakabidhi 😂😂 walale na magereza wao😂😂 Rest in peace 🕊️ rais wetu
@charlesmakuri792
@charlesmakuri792 5 жыл бұрын
Hawa wanajikosha kwa kina mbowe eti serikali iwape magodolo wafungwa,hivi uende gerezani utoke hujakelwa sasa hereza au umeenda kutalii ,jengeni makazi yenu
@Mwinamila-3
@Mwinamila-3 9 ай бұрын
N viongoz wachache wanaoweza kichukua maamuzi kama haya
@eliyawilliammagesamarwa8413
@eliyawilliammagesamarwa8413 5 жыл бұрын
Kura yangu
@thabitngangila8562
@thabitngangila8562 5 жыл бұрын
chuma cha pua ukizingua anakuumbua
@genimaige6023
@genimaige6023 5 жыл бұрын
kusema ukweli toka moyoni jeshi la magereza lijitathinini upya yani ni sawa na baba tkt nyumba anatoa maagizo ktk familia yake na hayatekelezeki kwa wakati, hata mm nimechukia hii ni aibu, kama pesa zipo tatizo ni nn?? 😄😄😄😄😄😄
@mashimbadeograthiasmathias8583
@mashimbadeograthiasmathias8583 5 жыл бұрын
Canal jenga Bila shida Ila hao MAGEREZA watapike hela hizo
@mussaramadhani-in1ci
@mussaramadhani-in1ci Жыл бұрын
Zmzm
А что бы ты сделал? @LimbLossBoss
00:17
История одного вокалиста
Рет қаралды 9 МЛН
pumpkins #shorts
00:39
Mr DegrEE
Рет қаралды 113 МЛН
Seja Gentil com os Pequenos Animais 😿
00:20
Los Wagners
Рет қаралды 26 МЛН
JPM ALIVYOWAKA KUHUSU MAKONTENA KUCHELEWA
8:38
Millard Ayo
Рет қаралды 357 М.
RAIS MAGUFULI AFANYA ZIARA YA KUSTUKIZA GEREZA LA UKONGA  mp4
34:13
RAIS DKT. MAGUFULI AKIWA NJIANI KUELEKEA JIJINI DODOMA
32:41
Ikulu Tanzania
Рет қаралды 100 М.
MPOKI MUHUDUMU / BROTHER KEY TAJIRI
30:27
BONGO LAND
Рет қаралды 157 М.
Ziara ya Rais Magufuli kwenye Bandari ya Dar es salaam
5:57
Millard Ayo
Рет қаралды 957 М.
Rais Magufuli afanya ziara ya ghafla Wizara ya fedha Nov. 6, 2015
14:29
А что бы ты сделал? @LimbLossBoss
00:17
История одного вокалиста
Рет қаралды 9 МЛН