Рет қаралды 211
Mheshimiwa Charles Makongoro Nyerere Mkuu wa Mkoa wa Rukwa amekabidhiwa Ofisi leo tarehe 23 Juni 2023 na Mheshimiwa Queen Cuthbert Sendiga ambaye kwa sasa ni Mkuu wa Mkoa wa Manyara. Awali Mheshimiwa Queen Sendiga (kushoto) alikuwa Mkuu wa Mkoa wa Rukwa kabla ya kuteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Mheshimiwa Makongoro(kulia).
Makabidhiano hayo yamefanyika mjini Sumbawanga na kushuhudiwa na Viongozi wa Chama cha Mapinduzi (CCM),Kamati ya Ulinzi na Usalama, Viongozi wa Dini, Balaza la waee,Wakuu wa Taasisi za Umma na Serikali na Watumishi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa.
Aidha Mhe Queen Cuthbert Sendiga Mkuu wa Mkoa wa Manyara mapema kabisa amefika Katika ofisi za Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Rukwa kusaliamiana na kuagana na viongozi wa Chama Mkoani Rukwa,Sendiga amewaomba kuendelea kutoa Ushirikiano wa Dhati kwa Mhe Charle Makongoro Nyerere ambaye ni Mkuu wa Mkoa wa Rukwa kama walivyofanya kwake kipindi akihudumu kama Mkuu wa Mkoa wa Rukwa