Salama Na MASOUD KIPANYA SE6 EP60 | HERI KUFA MACHO… PART 1 | SendTip MPESA LIPA NO 5578460

  Рет қаралды 72,835

YahStoneTown

YahStoneTown

Күн бұрын

#SalamaNa #SendTip Through MPESA #5578460
Habibi Masoud Kipanya ni Ally Masoud Nyomwa ambaye ni LEGEND. Kwa mujibu wake alizaliwa huku kakunja ngumi na dhana yake ni kwamba alizaliwa ili awe bondia! Kwa anacho kifanya na ambacho amekua akikifanya tena kwa ufasaha kwa miaka nenda miaka rudi bila ya shaka ni UBONDIA. Hakuna ambaye atabisha juu ya hilo. Amekua akipigania mambo tele na kuyasemea mengi pamoja na kuchekesha na kuelimisha kupitia kalamu yake. Kwa mujibu wake yeye ni mbobevu katika taaluma ya kupuuza na kuchukulia mambo poa kwa kipindi sasa. Lakini pia anaamini yeye ni MTATA. Tukienda mbele na kurudi nyuma, hapo kwenye UTATA hakuna ambaye anaweza kumbishia, hasa kwa wale ambao kalamu yake imewanyoosha kwa kiasi kikubwa.
Mimi na yeye tulikutana kwa mara ya kwanza takriban miaka kumi na tisa iliyopita, wakati huo mimi mbichi hasa na yeye akiwa kashajielewa na chemchem yake ya kipato tayari ilikua inatoa neema. Mimi nilikua ndo kwanza naanza kazi ya kujishikiza pale Times FM kipindi hiko bado ilikua kule Kamata. Masoud alikua analichorea gazeti la Majira ambalo lilikua liko kwenye mwamvuli mmoja na Radio ambayo nami nilikua nimejishikiza baada tu ya kumaliza skuli. Urafiki wetu ulikuja naturally tu maana sote tunapenda kucheka. Kupitia Zuhura Yunus na Binti mwengine wa kuitwa Rahma ndo mimi naye tulifahamiana. Wakati huo yeye alikua na gari kwahiyo lifti za hapa na pale zilikua hazikauki. Pia tulikua tunaitumia gari yake kama sehemu ya ku chill na kuskiliza muziki kwenye parking za Times FM.
Huwezi kukaa kwenye tasnia moja kwa muda mrefu kama wewe si hodari na mwenye kujielewa. Moja ya vitu ambavyo naviusudu kutoka kwake ni uelewa wake wa mambo tele wa tele, IQ yake ni ya juu sana na jinsi ambavyo ana reason ndo huwa anamaliza kabisa, kama binadamu wakati mwengine ni bora kukubaliana kuto kukubaliana na kwakwe yeye wakati mwengine jinsi anavyo wachora baadhi ya matukio na watu huwa haviishii kuzuri lakini hiyo haikuwahi kuwa sababu ya yeye kuacha kufanya ambacho anakifanya na ambacho amekua akikifanya kwa muda sasa. Uelewa wake kwenye mambo ambayo yanaendelea, uwezo wake wa kuona mbali na kuweka sanaa yake hiyo kwenye karatasi kisha kutuachia sisi tung’amue maana yake kwa kweli ni kipaji cha kipekee ya sana. Mmoja anatakiwa akae tu mbali na ku admire akifanyacho na hiko ndo ambacho mimi nimeamua kufanya.
Nilikua nataka anielezee maana halisi ya baadhi ya michoro yake ambayo iliacha gumzo kwa muda mrefu lakini kwa sababu ambazo niliziheshimu alisema asingependa iwe hivyo, uhuru wa kuwaacha watu watafsiri wao ndo raha ya kazi yake ingawa yeye anajua hasa kwanini alichora na maana yake hasa ni nini! Kwa heshima ya sanaa ilibidi nikubali matokeo. Toka umeanza kumjua na kufuatilia kazi yake, mara ngapi ushawahi kuskia Masoud yuko matatani? Yaani kakamatwa au hajulikani alipo? Kwangu mara kadhaa lakini haikuwahi kuwa kizuizi cha yeye kuacha kufanya afanyacho, kuogopa je? Nadhani kama binadamu kuwa na uoga ni jambo la kawaida, ila unafanyaje baada ya hapo ndo tofauti yetu.
Episode hii inajumuisha karibu yote ambayo niliwahi kutaka kumuuliza, mengine nilipata majibu nlotaka na mengine yalitolewa mbavuni, kwa ki vyovyote vile nili enjoy sana mimi na wenzangu na kutoka kwetu tunatumai nawe uta enjoy kama ambayo nasi tuli enjoy na kujifunza kutoka kwa MWAMBA huyu.
Love,
Salama.
Support us through anchor.fm/yahs...
SUBSRIBE TO OUR CHANNEL bit.ly/YahSton...
Listen our Podcast on
Spotify Link spoti.fi/2Uxr6Cm‬
‪ApplePodcast Link apple.co/2Ou1bru‬
GooglePodcast Link bit.ly/GoogleP...
Audiomack Link bit.ly/YahSton...
‪KZbin Link bit.ly/KZbinS...
Soundtrack Yeah by @MarcoChali • Marco Chali Feat One T...
Follow:
Twitter: / yahstonetown
Instagram: / yahstonetown
Facebook: / yahstonetown
Channel Administered by Slide Digital
Instagram: slidedigitaltz

Пікірлер: 93
@GivenTobago
@GivenTobago Жыл бұрын
Masoud aliwahi kunifundisha kuchora cartoon ilikua ni semina ya wikimbili kwa watoto wa shule ya msingi wenye vipaji vya uchoraji yalikua ni maswala ya usalama barabarani shule ya msingi Naura Arusha Central namshukuru sana nilipata basics nzuri juu ya comic na sasa nafanya Graphics web development na 3d graphics making big up to him.
@echolude
@echolude Жыл бұрын
From a Kenyan based in the states: Masoud has that rare quality of exuding wisdom without much affectation, a wisdom that is edifying & actually locally derived. Apwe Heshima Yake! The same can be states of Salama: a wise woman indeed without being off putting & hyperbolic.
@leylamohamed9939
@leylamohamed9939 Жыл бұрын
Masoud ni Kijana wa Sasa anayeishi mifumo ya Zamani, Birthday, Anniversary SIO ISHUUU... Safi sana 👊🏽👊🏽👊🏽
@emanualkadutu4130
@emanualkadutu4130 4 ай бұрын
Mzee huyo
@onlyacappellaallowed1743
@onlyacappellaallowed1743 Жыл бұрын
Salama unajua ya jufanya mahojiano mazito yawe kama 'kupiga stori' Big up sana
@aminanamoyo83
@aminanamoyo83 Жыл бұрын
We ❤ you masoud kwaajili ya Allah Asante Salama kwa kumleta kipenzi chetu ❤🙏🇹🇿🇨🇭
@joycembuya8480
@joycembuya8480 Жыл бұрын
Salama uu mwanamke jasiri na mwerevu sana Big up
@saumusalimuhassan2499
@saumusalimuhassan2499 Жыл бұрын
Nakukubali sana Masoud, sijawahi kukereka kwenye interview yako yoyote ile, bro Nakupenda sana 😘 *Masoud Kipanya*
@abdallahmdangadachi7030
@abdallahmdangadachi7030 Жыл бұрын
Sichoki kumuangalia Kipanya toka mkasi hadi Yah Stonetown bonge moja la kolabo Masoud na Salama
@frankissaya2578
@frankissaya2578 Жыл бұрын
I wonder why hizi doctorate za heshima hapewi Dr Kipanya
@carolineoyugi7771
@carolineoyugi7771 Жыл бұрын
Sa ajanunua atapewa vipi na umesikia watu wananunua😂😂😂
@ashurajengela3926
@ashurajengela3926 Жыл бұрын
Yani yuko very genius
@prudencemushi6948
@prudencemushi6948 Жыл бұрын
Nadhan busara ilitumika wakaona apewe Babu Tale kwanza
@DoctorPesandegeMgangaTibAsili
@DoctorPesandegeMgangaTibAsili Жыл бұрын
Tatizo mbahili mno huyu jamaa 😅
@Marjeby
@Marjeby Жыл бұрын
Masoud Kipanya ni akili kubwa sana wallah
@stanleymanimo769
@stanleymanimo769 Жыл бұрын
Wewe ni mtu poa sana masudi
@philemonpeter8973
@philemonpeter8973 Жыл бұрын
salama nimependa sana,maswali yako,na jinsi masoud kipanya anavyo jibu,maswali yako,natamani sana kujua jinsi ya kununua hisa
@joviangeofrey7212
@joviangeofrey7212 Жыл бұрын
Nafikir ni vyema utafute taarifa za makampuni mbalimbali. Kuna muda wanatangaza hiza
@agostineminde6025
@agostineminde6025 Жыл бұрын
Huyu jamaa anahitaji heshima yake 👍
@claratemba44
@claratemba44 Жыл бұрын
Ushauri mzuri sana
@abdulhamis9825
@abdulhamis9825 Жыл бұрын
Mwamba Kabsa, Mtu Makin Jamaa Ambaye Sijawah kuchoka Kumsikiliza Na Kujifunza Kutoka Kwake KP
@emmamatemu8225
@emmamatemu8225 Жыл бұрын
Umeandikaje hujaeleweka
@abdulhamis9825
@abdulhamis9825 Жыл бұрын
@@emmamatemu8225 typing error
@VictorChrispinSamson
@VictorChrispinSamson Жыл бұрын
Superb interview, never thought KP atakuwa down to earth like this.
@epiphaniaallute2726
@epiphaniaallute2726 Жыл бұрын
Asante Kaka Mosoud kuna jambo nimejifunza kupitia maelezo ya Malcom. Barikiwa sana kwa hili.
@Calky__-un5qd
@Calky__-un5qd Жыл бұрын
Nimependa sana brother Masoud,nimepata kitu❤️🔥
@fatmaahamadabass8080
@fatmaahamadabass8080 Жыл бұрын
Duh Allah amsameh huyo mtu unafurahiya maradhi ya mwenzio kweli
@mohdapper
@mohdapper Жыл бұрын
Pride of Africa Masoud kipanya
@florageofrey9486
@florageofrey9486 Жыл бұрын
Nimecheka sana kwakweli
@queenmaa30
@queenmaa30 Жыл бұрын
Kiukweli nimejifunza ktu...elimu nzuri sana
@salviusbasil5334
@salviusbasil5334 Жыл бұрын
Masoud arudishe ile #MaishaPlus
@jacklineabella7634
@jacklineabella7634 Жыл бұрын
I was waiting for this interview so badly.
@rehemaothman2475
@rehemaothman2475 Жыл бұрын
❤❤❤❤Nimejiona
@NGUFUSALOMI
@NGUFUSALOMI Жыл бұрын
Hilo cheko la Salama
@abuujuhayfa4321
@abuujuhayfa4321 Жыл бұрын
Mzee wa vipanya 🎉
@msafirimiracle6613
@msafirimiracle6613 Жыл бұрын
Haya bhana kwa hiyo mmeamua kurudi nyuma miaka,2022 😁
@bumbuli4170
@bumbuli4170 Жыл бұрын
Genius
@emilyrenatus9374
@emilyrenatus9374 Жыл бұрын
Kp 🗽
@sossyforreal814
@sossyforreal814 Жыл бұрын
Masoud is a very smart man aisee. Salama sasa tuletee Podcast.
@Stevematongo
@Stevematongo Жыл бұрын
Incredible interview.
@nurdinkarata7985
@nurdinkarata7985 Жыл бұрын
🔥🔥🔥
@franciskassanga7999
@franciskassanga7999 Жыл бұрын
nimeipenda hii, #siyo issue
@nepiasmwasanga1309
@nepiasmwasanga1309 Жыл бұрын
Kumbe wengine hawapeleki michango SHUBAMIT..😀😀
@nurdinkarata7985
@nurdinkarata7985 Жыл бұрын
Logic sister salama 👊🏻
@JanethKomba-tv7jy
@JanethKomba-tv7jy Жыл бұрын
Jamani tujifunze kupitia interview za ece jay not always tunataka kuona makosa t,ila we need to be strong bhna as broo kp did to handle Malcolm's issues
@albogastmselejr4583
@albogastmselejr4583 Жыл бұрын
Nilikuwa Naisubiliaa Kwa Muda Hii Interview 🏃🏃
@amytullah2175
@amytullah2175 Жыл бұрын
Hio ya makochi jamani hata mie nilishachanaa😅😅😅😅 daah!! Nilichezea zakufa mtu😅😅😅
@SeekerMaulid
@SeekerMaulid Жыл бұрын
Sister Salama Leo umecheka sana Jamani :), Huu sio 2022 ni 2023.
@godblessmwacha5201
@godblessmwacha5201 Жыл бұрын
ni ya muda kweli.. usidhani ni wamekosea. ivi vipindi vingi vya salama ni vya muda.
@tanzaniamycountry9308
@tanzaniamycountry9308 Жыл бұрын
Ahaaaa😀😀😀😀😀 salama bhana
@ramadhanimtetu3656
@ramadhanimtetu3656 7 ай бұрын
Kipanya Kama kipanya
@abdulhakimmwango9370
@abdulhakimmwango9370 Жыл бұрын
Leo ndo umeamua kuiachia si ndio😅😅😅 haya bwana master mind salama
@enockcharles6750
@enockcharles6750 Жыл бұрын
nimesubir sana hii yani
@joviangeofrey7212
@joviangeofrey7212 Жыл бұрын
Jaman kuna benk flan ilitaka kuanzishwa nikanunua hisa. Huu mwaka wa kumi sijapewa gawio. Inauma jmn
@issakitundu617
@issakitundu617 Жыл бұрын
et huu mwaka gani salama
@dansondannytv8111
@dansondannytv8111 Жыл бұрын
Salama ivi nikifikia level gani ya kimaisha naweza fanyiwa Interview na wewe
@leilaassey1726
@leilaassey1726 Жыл бұрын
Kumbe ya kitambo salama 22 tena
@hamyrhai9957
@hamyrhai9957 Жыл бұрын
Kipanya
@DemusTheGD
@DemusTheGD Жыл бұрын
huyu #Mzee Hanaga shidah.
@hustlaztv2352
@hustlaztv2352 Жыл бұрын
Nlijua dr harison 😅
@barakakusa7606
@barakakusa7606 Жыл бұрын
Masoud ni mwamba hasa ila nashangaa kwanini kwenye teuzi zinazofanywa wanamsahau, Ana kitu huyu 😂😂😂😂
@Jay47tz
@Jay47tz Жыл бұрын
Tuna hitaji elimu kwenye hisa
@sangomamourice3539
@sangomamourice3539 Жыл бұрын
Akili mingi mno mwamba hasa
@mactongathe179
@mactongathe179 Жыл бұрын
Apo kweny family dah nmechKaaa saNaa Brooo kipaNya! Birthday na hio namba yao Dah! But ....
@richardcastromzena5136
@richardcastromzena5136 Жыл бұрын
13:30 😂 16:10 😂 19:52 22:40 kaka imara sana
@godblessmwacha5201
@godblessmwacha5201 Жыл бұрын
kumbe ni ya mwaka 2022? Dah
@barakawiseman5073
@barakawiseman5073 Жыл бұрын
Masudi anamuonekano wa umwakyembe flani ivi
@mohamednaaman188
@mohamednaaman188 Жыл бұрын
2022 😀
@romes-tz7323
@romes-tz7323 Жыл бұрын
Mwamba wamda marefu like kwake👊
@faudhiasalum7279
@faudhiasalum7279 Жыл бұрын
✌️✌️
@dengahmediatz3113
@dengahmediatz3113 Жыл бұрын
Tunatak interview yak salama
@TungoTamu2756
@TungoTamu2756 Жыл бұрын
Yan apatikane mtu wa kumuhoji vizuri kama yeye anavyowahoji wengine
@mr.theoswahiliteacher.
@mr.theoswahiliteacher. Жыл бұрын
Watu wawili wenye IQ kubwa wamekutana.
@Yusufu940
@Yusufu940 Жыл бұрын
Salma ume una ma swali 😮
@abdulnaseermrisho4342
@abdulnaseermrisho4342 Жыл бұрын
😂😂😂😂 Masoudy kama Masoudy
@philomenamushi5606
@philomenamushi5606 Жыл бұрын
Shubaamiti😝hapo ndo kashatukana
@joesimba
@joesimba Жыл бұрын
17:00 hizi interview nyingine zilifanyika mwaka jana nini.
@brightvatta284
@brightvatta284 Жыл бұрын
Yawezekana naona pia mtangazaji kasema 2022
@peterkichochi7510
@peterkichochi7510 Жыл бұрын
Miaka imeridi nyuma mwaka 2022😂😂😂😂
@nzumbimasanja
@nzumbimasanja Жыл бұрын
Wanarekodi kisha wanapandisha muda wowote. Hii ni ya zamani
@godfreymiho4927
@godfreymiho4927 Жыл бұрын
Making sana,jamaa alinifany nipend kuchor
@philomenamushi5606
@philomenamushi5606 Жыл бұрын
🤔😂salama hii ni 2022😓🤔realy😳👀😳hii ni 2023 tafadhali✋🏿
@highmanjerry9640
@highmanjerry9640 Жыл бұрын
Kipindi kilisha recodiwa mzee kama ww ni mfatiliaji kwa tv ungesha jua,humu kwa youtube huwa wanaweka baada ya kuonekana kwa tv kwhyo walio kosa show kwa tv basi utakutana nayo huku
@charlesolomi9514
@charlesolomi9514 Жыл бұрын
Interview yooteee umeona hilo kosa tu
@Hashdough
@Hashdough Жыл бұрын
OPENING YA KIBABE KABISA
@leonarddamian
@leonarddamian Жыл бұрын
Sana
@godsonmunisi7229
@godsonmunisi7229 Жыл бұрын
Interview was badly .salama anakuuliza swali .but swali halijibu anatoa maelezo mengi sana nje ya swali.
@piuslwinga6233
@piuslwinga6233 Жыл бұрын
Utakuwa unachuki zako tu
@godsonmunisi7229
@godsonmunisi7229 Жыл бұрын
I know you was want to act like genius. But wasn't what happens like you was wish .try to listen question carefully before answering questions
@frankkajoba8372
@frankkajoba8372 7 ай бұрын
Tatizo kujifanya "much know" kiingereza gani hicho sasa wewe chizi? Hujui chochote kipindi kama hiki hakikufai kasikilize singeli ndio saizi yako.
@blandinamyinga9489
@blandinamyinga9489 Жыл бұрын
""anivesari""???🤣🤣🤣🤣🤣@masoudkipanya🙌🙌🙌🙌
Каха и дочка
00:28
К-Media
Рет қаралды 3,4 МЛН
Сестра обхитрила!
00:17
Victoria Portfolio
Рет қаралды 958 М.
ABIUD AMLIZA RITHA, ANAJUA KUIMBA SANAA.
4:50
Nyota Shine Tv
Рет қаралды 1,8 М.
MASOUD KIPANYA KUHUSU KUKATAA UTEUZI "UTEUZI AKIKUPA MUNGU,TUNAJISHUSHA MNOO, UNAWEZA UKACHEKA"
56:35
Mchezakwao “mchezakwaoshow” Startv
Рет қаралды 5 М.