No video

Salama Na MASOUD KIPANYA SE6 EP60 | HERI KUFA MACHO… PART 2 | SendTip MPESA LIPA NO 5578460

  Рет қаралды 40,137

YahStoneTown

YahStoneTown

Күн бұрын

#SalamaNa #SendTip Through MPESA #5578460
Habibi Masoud Kipanya ni Ally Masoud Nyomwa ambaye ni LEGEND. Kwa mujibu wake alizaliwa huku kakunja ngumi na dhana yake ni kwamba alizaliwa ili awe bondia! Kwa anacho kifanya na ambacho amekua akikifanya tena kwa ufasaha kwa miaka nenda miaka rudi bila ya shaka ni UBONDIA. Hakuna ambaye atabisha juu ya hilo. Amekua akipigania mambo tele na kuyasemea mengi pamoja na kuchekesha na kuelimisha kupitia kalamu yake. Kwa mujibu wake yeye ni mbobevu katika taaluma ya kupuuza na kuchukulia mambo poa kwa kipindi sasa. Lakini pia anaamini yeye ni MTATA. Tukienda mbele na kurudi nyuma, hapo kwenye UTATA hakuna ambaye anaweza kumbishia, hasa kwa wale ambao kalamu yake imewanyoosha kwa kiasi kikubwa.
Mimi na yeye tulikutana kwa mara ya kwanza takriban miaka kumi na tisa iliyopita, wakati huo mimi mbichi hasa na yeye akiwa kashajielewa na chemchem yake ya kipato tayari ilikua inatoa neema. Mimi nilikua ndo kwanza naanza kazi ya kujishikiza pale Times FM kipindi hiko bado ilikua kule Kamata. Masoud alikua analichorea gazeti la Majira ambalo lilikua liko kwenye mwamvuli mmoja na Radio ambayo nami nilikua nimejishikiza baada tu ya kumaliza skuli. Urafiki wetu ulikuja naturally tu maana sote tunapenda kucheka. Kupitia Zuhura Yunus na Binti mwengine wa kuitwa Rahma ndo mimi naye tulifahamiana. Wakati huo yeye alikua na gari kwahiyo lifti za hapa na pale zilikua hazikauki. Pia tulikua tunaitumia gari yake kama sehemu ya ku chill na kuskiliza muziki kwenye parking za Times FM.
Huwezi kukaa kwenye tasnia moja kwa muda mrefu kama wewe si hodari na mwenye kujielewa. Moja ya vitu ambavyo naviusudu kutoka kwake ni uelewa wake wa mambo tele wa tele, IQ yake ni ya juu sana na jinsi ambavyo ana reason ndo huwa anamaliza kabisa, kama binadamu wakati mwengine ni bora kukubaliana kuto kukubaliana na kwakwe yeye wakati mwengine jinsi anavyo wachora baadhi ya matukio na watu huwa haviishii kuzuri lakini hiyo haikuwahi kuwa sababu ya yeye kuacha kufanya ambacho anakifanya na ambacho amekua akikifanya kwa muda sasa. Uelewa wake kwenye mambo ambayo yanaendelea, uwezo wake wa kuona mbali na kuweka sanaa yake hiyo kwenye karatasi kisha kutuachia sisi tung’amue maana yake kwa kweli ni kipaji cha kipekee ya sana. Mmoja anatakiwa akae tu mbali na ku admire akifanyacho na hiko ndo ambacho mimi nimeamua kufanya.
Nilikua nataka anielezee maana halisi ya baadhi ya michoro yake ambayo iliacha gumzo kwa muda mrefu lakini kwa sababu ambazo niliziheshimu alisema asingependa iwe hivyo, uhuru wa kuwaacha watu watafsiri wao ndo raha ya kazi yake ingawa yeye anajua hasa kwanini alichora na maana yake hasa ni nini! Kwa heshima ya sanaa ilibidi nikubali matokeo. Toka umeanza kumjua na kufuatilia kazi yake, mara ngapi ushawahi kuskia Masoud yuko matatani? Yaani kakamatwa au hajulikani alipo? Kwangu mara kadhaa lakini haikuwahi kuwa kizuizi cha yeye kuacha kufanya afanyacho, kuogopa je? Nadhani kama binadamu kuwa na uoga ni jambo la kawaida, ila unafanyaje baada ya hapo ndo tofauti yetu.
Episode hii inajumuisha karibu yote ambayo niliwahi kutaka kumuuliza, mengine nilipata majibu nlotaka na mengine yalitolewa mbavuni, kwa ki vyovyote vile nili enjoy sana mimi na wenzangu na kutoka kwetu tunatumai nawe uta enjoy kama ambayo nasi tuli enjoy na kujifunza kutoka kwa MWAMBA huyu.
Love,
Salama.
Support us through anchor.fm/yahs...
SUBSRIBE TO OUR CHANNEL bit.ly/YahSton...
Listen our Podcast on
Spotify Link spoti.fi/2Uxr6Cm‬
‪ApplePodcast Link apple.co/2Ou1bru‬
GooglePodcast Link bit.ly/GoogleP...
Audiomack Link bit.ly/YahSton...
‪KZbin Link bit.ly/KZbinS...
Soundtrack Yeah by @MarcoChali • Marco Chali Feat One T...
Follow:
Twitter: / yahstonetown
Instagram: / yahstonetown
Facebook: / yahstonetown
Channel Administered by Slide Digital
Instagram: slidedigitaltz

Пікірлер: 102
@peterlujuo1640
@peterlujuo1640 Жыл бұрын
Ukiitoa show ya ruge kwenye mkasi, hii ndo show bora ya salama, mahojiano yenye contents. Nime enjoy na kujifunza big up y'all
@veridianacharles4511
@veridianacharles4511 Жыл бұрын
Masoudy ni kama muda wake ulikuwa mdogo ilifaa aendelee kutuambia mambo mengi zaidiiii ....... nimejifunza I wish maisha plus irudi tena
@msunjigfx8644
@msunjigfx8644 Жыл бұрын
This is the one of the Greatest Man in the World, pengine hatukumwaga damu back in a days kipindi cha uhuru, ama pengine amani tuliyonayo inatufanya tunarelax na kujisahau but INAWEZEKANA
@cheka480
@cheka480 Жыл бұрын
indeed
@2116-n
@2116-n Жыл бұрын
Hilo swali la "Tanzania yako unaiona wapi" majibu yake aiseeee, ni akili ya kiwango Cha juu Sana🙏🙏🙏🙌
@philomenamushi5606
@philomenamushi5606 Жыл бұрын
Hakika nimejifunza vitu vingi na ninazidi kujifunza 🤲🙏salama 🤲🙏masoudy🤲🙏asantee kwa darasa
@aloycemwambwiga2318
@aloycemwambwiga2318 Жыл бұрын
Salama J! Kipindi chako kinaelimisha, kinajenga ujasiri, kinakuza kiimani. Nawe Mungu akuweke kama ulivyomwambia Masoud
@JohnMadaba-gb1je
@JohnMadaba-gb1je Жыл бұрын
Salama kama unahitaji kujua uwekezaji was hisa na Hati fungani niambie. Ntakusaidia elimu for free. I am your fan
@lutufyojason2598
@lutufyojason2598 Жыл бұрын
Kaka John .naomba uniongeza na mimi
@gracepaulo704
@gracepaulo704 Жыл бұрын
Namm nahtaj weka no bro
@joshuamacha8751
@joshuamacha8751 Жыл бұрын
Mimi nataka kujua pia
@mrfashion1687
@mrfashion1687 Жыл бұрын
Kali sana hii na nilikua naisubiri hongera kwa kutuletea huyu mtu, sasa bado SALAMA NA MILLARD AYO
@frankphiri2666
@frankphiri2666 Жыл бұрын
This guy is one of a kind my best quote "mnanunua hela mnapata wapi" kama nyie ni consumers na si producers
@STEPHENJUSTINE-ty4nh
@STEPHENJUSTINE-ty4nh Жыл бұрын
Mtu muhimu sana kwenye taifa letu na maisha ya WaTanzania ...💯🔥
@alifocusmsham7623
@alifocusmsham7623 Жыл бұрын
Yani intrerview imeisha wakati ndokwanza inataka kuanza
@jerrymwakapemba5644
@jerrymwakapemba5644 Жыл бұрын
Nakupenda sana Masoud, huwa sichoki kukusiliza. MUNGU azidi kukutunza, una vitu vingi sana kwa ajili ya kuisadia jamii yetu (nchi yetu). Salama, nakupenda pia, kipindi chako kina mambo mengi sana ya muhimu kwetu. Big up you all!
@saumusalimuhassan2499
@saumusalimuhassan2499 Жыл бұрын
Mungu akupe umri mrefu na Afya NJEMA Masoud Wetu 🙏
@businesstanzania
@businesstanzania Жыл бұрын
Masoud Amezaliwa Zama Ambazo Sio Zake, Atusamehe Bure, Tukitaka Kumuelewa Tumpe Nchi.
@Curioustraveller254
@Curioustraveller254 Жыл бұрын
Watu wasikujue saana...Familiarity breeds contempt Masoud nailed that
@Bob-kz2ql
@Bob-kz2ql Жыл бұрын
Strong heart Boss Kipanya, hiyo mentality wachache sana wanazo hasa wababa so tumejifunza mamb mengi sana hapo hasa sisi wanaume…be blessed Salama zaidi tupe watu makini sio wale channel za udaku na kutafuta umbea😂😂
@mwandamboevans-wj8kp
@mwandamboevans-wj8kp Жыл бұрын
Shukran sana Kwa hichi Sister Salama,mbalikiwe sana na muishi sana
@mwengmfaume5301
@mwengmfaume5301 Жыл бұрын
Nilikuwa nampenda malkom tangu akiwa mdogo japo nilikuja kumuona akiwa amekuwa kuwa,nakumbuka nilikuwa ndo kabinti niliuwa sipitwi na kipindi cha wàtoto chuchuchu , kaka masood na malkom,marehem Amina chifupa na rahmani,,yaani nino, na kaka bonda yey hakuwa na mototo walikuwa wakimcheka kimatani,,aisee
@gtunewaves2867
@gtunewaves2867 4 ай бұрын
masoud anaongea vizuri na kwa ufasaha sana
@rm9756
@rm9756 Жыл бұрын
Plz Salama tuna muitaji tena japo 2hrs tu maana Ana vingi vya kutufunza From Kansas in USA 🤜🏿🤛🏿
@veridianacharles4511
@veridianacharles4511 Жыл бұрын
Niliona kama kuna mengi tunahitaji kujifunza toka kwake
@salamisindimwo303
@salamisindimwo303 Жыл бұрын
Kipindi kizuri...shukran kwa Mtangazaji,shukran kwa mgeni Ustadh Msoud...tumenufaika na kufaidika piya kupitiya mazungumzo yenu...
@kamuchidyblez2136
@kamuchidyblez2136 Жыл бұрын
God bless you masoud wewe ni genius sana aise naamn watu walio karibu na wewe kuna vitu vingi sana wanavipata kutoka kwako ,pia nikupongeze sana salamaa uko smart kwenye kazi yako #greatinterview
@mfaumejuma2375
@mfaumejuma2375 Жыл бұрын
What an Interview.....Absolutely Sensational!
@lukullikiwamba6494
@lukullikiwamba6494 Жыл бұрын
Masud kipanya ni Kati ya watu wenye fikra nyingi sana katika nchi ya Tanzania na bara lake sema sisi watu weusi tumeloga na aliyetuloga kafa, watu Kama yeye uwa tunawachukulia kawaida sana …… mungu ampe maisha marefu kaka yetu kwani bado ana mambo mengi sana kutujuza toka kwenye kichwa chake, Salama sina mengi ya kusema juu yako , you one of the best interview ever live in our generation, was good talk I love it
@hellenmroso6786
@hellenmroso6786 Жыл бұрын
Hiii show imekuwa fupi sana. "Tafuta taarifa upate maarifa"
@glorykileo8601
@glorykileo8601 Жыл бұрын
Vp ile show ya maisha plus bonge moja la show itufunza mambo mengi sana kama vijana tunaihitaji tafafhali
@petermadokola7625
@petermadokola7625 Жыл бұрын
Masoud I'm 55years, I studied mechanical engineering, based to motor vehicle, for over 30year, you inspires me big time, man you have great mind weather we want it or not but the truth stand still, Is there any chance we can meet, I would say we are some way alike, I'm a practically man ,you won't regret lay the table with me,
@giftwieland6322
@giftwieland6322 Жыл бұрын
There is very thin line between love and hate🔥
@alifocusmsham7623
@alifocusmsham7623 Жыл бұрын
Huwa sikuzote simalizi kiu yangu ya kumsikiliza Masoud, nimeangalia interview zake nyingi sana lakini bado nataka zaidi na zidi.
@abdulhakimmwango9370
@abdulhakimmwango9370 Жыл бұрын
Kuna content mmezikata na zilikuwa zinaumuhimu mno sanjari na Hilo bado show ni Kali mashaallah
@priscajonas7805
@priscajonas7805 Жыл бұрын
Daaaaah nimejifunza kitu kikubwa Sana thank brother 🙏
@enockcharles6750
@enockcharles6750 Жыл бұрын
salama si haki hii ya mwaka jana iruduwe bwana
@faridaissa909
@faridaissa909 Жыл бұрын
This is the best asante sana salama 🙏
@josegisbert4351
@josegisbert4351 Жыл бұрын
Naomba umuhoji Masoud kila siku...
@joycembuya8480
@joycembuya8480 Жыл бұрын
🤣
@emerensianamaganza8322
@emerensianamaganza8322 Жыл бұрын
Hawa ndo watu wa kuwekwa serikalini walete elimu na mabadiliko katika jamii, siyo tuu watu watuuu
@UgandanAllstarTales
@UgandanAllstarTales Жыл бұрын
SHIRT LAKE KALI SANA
@egbertpesha4082
@egbertpesha4082 Жыл бұрын
Great interview. Thought-provoking. Masoud has a big mind.
@allenmanzi9869
@allenmanzi9869 11 ай бұрын
Safi sana Masoud. Hapo kwenye Business Plan. Ni Ukweli Mchungu. very true.
@Mfundo272
@Mfundo272 Жыл бұрын
Ningefurahi sana Kama nitapata namba ya Kipanya, from Germany
@maridadi_2g
@maridadi_2g Жыл бұрын
Men 🎉 Big up to Masoud I like your critical thoughts. Asante salama
@ayubustanley9069
@ayubustanley9069 Жыл бұрын
NAWAKUBALI SANA.NBRO.masoud Kipanya nakukubali sana
@mwajabumalekela5563
@mwajabumalekela5563 Жыл бұрын
Duuuuhhh!! Nimejifunza kitu kikubwa saaana, hongera sana cis Salama na big up kaka Masoud, Mungu aendelee kukuweka na kile kilichopo ndani kiendelee kumea
@raheemkareem8055
@raheemkareem8055 Жыл бұрын
Super genius🔥
@aminanamoyo83
@aminanamoyo83 Жыл бұрын
❤ masoud, thanks Salama but please mrudishe tena tafadhali 🙏🇹🇿🇨🇭
@georgemuigai7427
@georgemuigai7427 Жыл бұрын
Hakika nimejifunza kitu kwa brother masoud,Mimi nataka kitabu nitakipata wapi?
@abdulhamis9825
@abdulhamis9825 Жыл бұрын
Rais Anateua Watu Kushika Nyadhifa MbaliMbali Katika Serikal Na Maeneo Ya Nchi Lkn Iman Yngu Mpka Leo Bado Hajajua Ww Utashka Nafas Gani Ww Ni GENIUS
@martinmhando8351
@martinmhando8351 Жыл бұрын
Genius Masoud.
@petermadokola7625
@petermadokola7625 Жыл бұрын
I have worked for 30 years I did different kind of innovation, at the meantime I'm thinking of working with sustainable agriculture based to irritation, your a philosopher,
@rehemarwanda6039
@rehemarwanda6039 Жыл бұрын
I love Masoud Kipanya huyu jamaa ana akili nyingi sana
@brownngullo4051
@brownngullo4051 Жыл бұрын
Masoud akili nyingi sana.. very inspired
@fredgrapher9838
@fredgrapher9838 Жыл бұрын
Masoud, my faviurite presenter…since Chuchuchu ya Clouds fm, power breakfast…you are genius
@dianerditto
@dianerditto Жыл бұрын
Hili ni darasa huru nimechukua point za kutosha sana leo, ahsante.
@barengayabomiriam
@barengayabomiriam Жыл бұрын
Yaani baba Malcolm iko kama Mimi simtu wamarafiki.naninapenda saaaana kuka pekeangu kwa sababu Mimi nafkiria saaaaaaaana
@GAVANA-ut2ek
@GAVANA-ut2ek Жыл бұрын
Masoud amebarikiwa IQ kubwa..! Best Interview 🙏
@bakarishaha7331
@bakarishaha7331 Жыл бұрын
hua namuelewa sana huyu jamaa. (kipanya) ni moja ya hazina , well done , please tuletee kaimu shehe wa mkoa DSM.
@emanuelsolomoni7003
@emanuelsolomoni7003 Жыл бұрын
Let me challenge Masoud, Dubai leo ina mafuta na utalii hela wanapata huko as Nation, Urussi ina Gas na Mafuta inapata fedha hapo, sisi tuna Gas, Madini, Utalii how we optimise these resources ziwe na tija kwa Taifa huoni kuna sehemu hatuko sawa, our Gvt needs to be Rich enough tukifika hapo itakuwa simple wao kufacilitate hizo manufacturing ma exports na kuleta Technology mpya, Serikali kama hela ya budget yake ni mpaka itafutane hatufiki, hiyo china, Marekani, Urussi, hata urabuni serikali zao zina hela nyingi sana kwakuwa ni wakali na wamesimamia ukweli kwenye resources zao!!
@abdallahmakombo3866
@abdallahmakombo3866 Жыл бұрын
Shida kuu Kwa nchi zetu ni , Elimu na ufahamu, Tumekosa elimu na ufahamu Kwa viongozi,mtu mmoja mmoja na jamii zetu, Hizo nchi uzitajazo Zina technology, knowledge, Ufahamu huo huwapa , Mawazo, ambayo huwatafuta watu sahihi Kisha hao watu huwapa mtaji / capital ambayo huleta kutatua changamoto za kidunia Kisha hupata zawadi( fedha nyingi/ THAMANI zaidi. Kwa hiyo Kuna haja kubwa ya kuwekeza kwenye wazo ( maarifa)Kisha technology ( mifumo ya uzalishaji Mali kisasa ,na ndipo tufike mbali ,HUKU TUKIJUA UJASUSI WA KIUCHUMI KIMATAIFA . Bado sana
@glorykileo8601
@glorykileo8601 Жыл бұрын
Nimependa hapo kwa rafiki
@heriethalexander5145
@heriethalexander5145 Жыл бұрын
This is hands down the best interview I have listened to tangu hii show ianze
@AmonAmon-bn6vn
@AmonAmon-bn6vn Жыл бұрын
Akili hzi za masoud Hawa ndio ilitakiwa wawepo bungeni,bahati mbaya wapo Africa.
@mhangwacastory8765
@mhangwacastory8765 Жыл бұрын
Ruge Mutahaba, Masoud kipanya ,Massanja,Zembela, Roma mkatoli ,Nauka nafikiri Hawa jamaa Tanzania inabidi iwatumie sana!
@charlesmasesa89
@charlesmasesa89 Жыл бұрын
Masud nakukubali na kunakitu chakujifunza toka kwako
@dullywa9973
@dullywa9973 Жыл бұрын
only content in this mahojiano 🎉
@2116-n
@2116-n Жыл бұрын
12:10,🤣🤣🤣🤣🙌🙌🙌, magari siyo matikiti au siyooo😂😂
@mucci_AI
@mucci_AI Жыл бұрын
Duuh bonge la interview
@Muuaah
@Muuaah Жыл бұрын
Voice over artist
@maximillianmasangya4784
@maximillianmasangya4784 Жыл бұрын
Nimejifunza shukran sana kwenu
@naziakijangwa983
@naziakijangwa983 Жыл бұрын
Makini broo❤❤
@ishakafaki3501
@ishakafaki3501 Жыл бұрын
Salma na ston town show naomba mniruhusu nitukane ili kiongozii wetu ajee hapa kumsikiliza huyu Kaka 😢😭😭😭
@katikatisafaris
@katikatisafaris Жыл бұрын
Big brother is not a show to impact an African community, nothing in there. May Allah make it easy for Kipanya to continue with MaishaPlus
@raimajimoto1122
@raimajimoto1122 Жыл бұрын
Nakukubali kaka
@yohanacosmasmachalila9016
@yohanacosmasmachalila9016 Жыл бұрын
Big up brother Masoud na dada yetu Salama
@lowkeybongo
@lowkeybongo Жыл бұрын
Masoud mtu special
@mungonyamilambo1157
@mungonyamilambo1157 Жыл бұрын
Bonge la interview 👏👏👏
@nevilekileo8262
@nevilekileo8262 Жыл бұрын
Nasubiria salama na Roma mkatoliki, salama na Kala Jeremiah
@richardmweusi6261
@richardmweusi6261 Жыл бұрын
Asaalaam Alleykum naomba utuletee na ezden jumanne!
@fundiseremalamohammedmdoe3711
@fundiseremalamohammedmdoe3711 Жыл бұрын
Masoud kipanya atafutwe tena, bado hajakata kiu yetu kama watazamaji
@MwanaidChomba-wx7ty
@MwanaidChomba-wx7ty Жыл бұрын
Maisha plus ingerudi Tena
@Emiliana97
@Emiliana97 Жыл бұрын
Big brains maahn🙏
@pauldmajo6827
@pauldmajo6827 Жыл бұрын
On Podcast is 2 good hours, this is summarized.
@mmn7480
@mmn7480 Жыл бұрын
Mi napenda tu slama tabasam lake
@abdallahmakombo3866
@abdallahmakombo3866 Жыл бұрын
Hakika, SISI WA TANZANIA NI WACHUUZI KABISA. BIDHAA ILIOTENGENEZWA NA MWINGINE HALAFU UNANUNUA ILI KUUZA KWA FAIDA
@jacksonndabhisiye4848
@jacksonndabhisiye4848 Жыл бұрын
kitabu chake kinaitwaje na kinapatikana wapi
@dnewztz
@dnewztz Жыл бұрын
12:13 utemgenezaji wa magari sio kilimo cha matikiti😉😉
@manstiko5890
@manstiko5890 Жыл бұрын
Usimruhusu mtu akakujua kuna siku atakutumia vibaya sana kukujua kwako
@ramadhanijuma9655
@ramadhanijuma9655 Жыл бұрын
Wakwanza
@mcrramon4649
@mcrramon4649 Жыл бұрын
Moja kati ya watu ambao wanafanya nijivunie kua Mtanzania
@News6Tz
@News6Tz Жыл бұрын
Natamani sana kama utakuwa unaleta watu wahivi wengi kuliko ambao hawana uwezo mkubwa wa kuzungumza vitu sensitive kama hawa mkifanya hivi wallah mtafika mbali hata vipindi vyenu kuwa namba 1 tanzania kuliko channel nyingi za hovyo cause hapa kuna vitu vingi vya kujifunza
@araphatywanyamale6475
@araphatywanyamale6475 Жыл бұрын
Why wasimpee aat uongoziii uyu jamaaaa ... mee naaminii iii Dhahabu kwa watanzaniaa aseee
@dengahmediatz1230
@dengahmediatz1230 Жыл бұрын
Jmn mahojiano mbn mafupi
@jobbyandrew4313
@jobbyandrew4313 Жыл бұрын
wa pili
@mwanaidimohamed9200
@mwanaidimohamed9200 Жыл бұрын
Watatu
@reinatave780
@reinatave780 Жыл бұрын
I wish Maisha plus Ingerud tena ngoja tuendelee kuomba dua
@erickmorro8852
@erickmorro8852 Жыл бұрын
Startup is hassling 🛺💪🏿, asante sana KP
@erickmorro8852
@erickmorro8852 Жыл бұрын
eMo Bodaboda Tanzania
Yummy Lifehack 😋 @artur-boy
00:19
Andrey Grechka
Рет қаралды 4,5 МЛН
Zombie Boy Saved My Life 💚
00:29
Alan Chikin Chow
Рет қаралды 33 МЛН
He bought this so I can drive too🥹😭 #tiktok #elsarca
00:22
Elsa Arca
Рет қаралды 43 МЛН
Mkasi - S01E03 Masoud Kipanya
25:38
MkasiTV
Рет қаралды 113 М.
MAHOJIANO KATI YA MASOUD KIPANYA NA PROF. MOHAMED JANABI KUHUSU UVIKO 19 PAMOJA NA CHANJO
1:33:25
Benjamin William Mkapa Foundation.
Рет қаралды 9 М.