Рет қаралды 691
Waziri wa Mambo ya Ndani Hamad Masauni amelipongeza jeshi la polisi kwa kuendelea kuhimarisha hali ya usalama nchini ambapo amesema kwa kipindi cha mwisho wa mwaka ajali zimepungua na matukio ya uhalifu kwa mwaka mzima yamepungua.
‘'Nalipongeza jeshi la polisi kwa kuweza kudhibiti ajali za barabarani ambazo zilifululiza kidogo kipindi cha katikati, Kipindi cha mwisho wa mwaka ajali zimepungua, Hata matukio ya uhalifu kwa ujumla siyo tu mwisho wa mwaka kwa muda wa mwaka mzima hali ya usalama katika nchi imeendele kuhimarika’'
Masauni amesema hayo leo Januari 4, 2023 wakati akizungumza na waandishi wa Habari Jijini Dar es Salaam.