Рет қаралды 949
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam imepanga kutoa uamuzi Jumatatu ya Septemba 23, 2024 wa dhamana ya aliyekuwa meya wa zamani wa Ubungo, Boniface Jacob, maarufu Boni Yai.
Uamuzi huo utatolewa baada ya upande wa mashtaka leo Alhamisi, Septemba 19, 2024 kumfikisha mahakamani na kumsomea mashtaka mawili.
Mbali na mashtaka hayo, awali waliomba Mahakama uzuie dhamana yake kwa muda. Hatua hiyo imeibua mabishano ya kisheria kati ya mawakili wa upande wa Serikali na wale wa Boni Yai.
Mchuano huo wa mawakili wa kila upande kutetea hoja zake umehitimishwa na Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakaka ya Kisutu, Franco Kiswaga anayesikiliza kesi hiyo kusema atatoa uamuzi Jumatatu ya Septemba 23, 2024, saa 5:00 asubuhi. Boni Yai amepelekwa mahabusu.
Mashtaka yanayomkabili Boni Yai likiwemo la kuchapisha taarifa za uwongo kwenye mtandao wake wa X (zamani Twitter), ambayo ameyakana.
Pia, Serikali ikawasilisha maombi mawili, kwanza mahakama imuamuru aruhusu vifaa vyake vya kielektroniki pamoja na akaunti yake ya X ili mpelelezi aweze kuviingilia na kuvifanyia uchunguzi.