Рет қаралды 203,956
Aliwaambia mamia ya wananchi waliokuwa wakimsikiliza kuwa amepata habari kuwa baadhi ya Wapemba wangependa mgombea Urais wa Zanzibar awe Seif Sharif Hamad (kwa wakati huo Maalim Seif alikuwa Waziri Kiongozi wa Zanzibar ambaye ni mzaliwa wa Pemba), badala ya Abdulwakil ambaye aliteuliwa na Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM.
Abdulwakil alichaguliwa kuwa mgombea pekee wa Urais wa Zanzibar baada ya kupata kura 85 ikilinganishwa na kura 78 za Maalim Seif.
“Halmashauri Kuu ya Taifa ingemchagua Hamad, nina hakika kungekuwa na mgogoro Unguja,” alisema Mwalimu Nyerere.