Рет қаралды 4,616
Wafanyabiashara wa maduka ya jumla na rejareja wilayani Handeni mkoani Tanga wamefunga maduka yao kutwa nzima wakidai kutolewa lugha za vitisho na Meneja wa Mamlaka ya Mapato Tanzania wilayani hapa, wakati wanapofika ofisini kwake.
Wakizungumza kwenye mkutano na kamati ya ulinzi na usalama katika kikao kilichofanyika viwanja vya Handeni Square, wafanyabiashara hao wamesema shida kubwa wanayokutana nayo TRA, ni lugha za vitisho kutoka kwa meneja na makadirio ya kodi ambayo si rafiki kwao.
Akijibu shutuma hizo, Meneja wa TRA wilayani Handeni, Venance Ephraim amesema changamoto iliyopelekea hali hiyo ni wafanyabiashara wengi kukosa elimu ya kodi na waliowengi hawataki kutoa risiti.