ZIARA YA UKAGUZI WA MIRADI YA MAENDELEO YA JIJI LA DAR ES SALAAM MANISPAA YA TEMEKE

  Рет қаралды 4,855

Mwananchi Digital

Mwananchi Digital

Күн бұрын

Bodi ya wakurugenzi wa DMDP(Dar es salaam Metropolitan Development project ) ikiwa katika ziara ya siku 2 yaani tarehe 7 na 8 oktoba 20202 kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo kwa jiji la Dar es salaam), ambayo inasimamiwa moja kwa moja na ofisi ya Rais TAMISEMI,kupitia TARURA (Tanzania Rulal and Urban Road Agency), ambayo imepangwa kutekelezwa kwa awamu mbili yaani 2015/20 na 2020/25 katika Manispaa tatu yaani Temeke,Ilala na Kinondoni.
Miradi hiyo imeghalimu kiasi cha pesa zaidi ya billion 600 kwa manispaa zote, ikiwa miradi hiyo inatekelezwa kwa fedha za mkopo wa serikali kutoka benki ya dunia.
Bodi hiyo ilifanya ziara yake ya kwanza katika manispaa ya Temeke, tarehe 7 octoba 2020 kwa kukagua miradi mbalimbali ya miundo mbinu ya kijamii ikiwemo barabara, masoko, mifereji na vituo vya Afya.
Halmashauri ya manispaa ya Temeke wamenufaika na miradi hiyo kwa kupata masoko 3 yaliyokamilika na kuanza kutumika kati ya masoko 6 yaliyo katika mradi huo, ikiwemo soko kubwa la kisasa lilopo Kijichi pamoja na stendi ya mabasi kijichi, vilevile ujenzi wa barabara zinazowaunganisha wakazi wa eneo hilo ikwa ni pamoja na barabara ya Kijichi kwenda Toangoma yenye urefu wa kilomita 3.2 na barabara ya mwanamtoti yenye km 1.8.
Miradi mingine ni ujenzi wa mifereji ya maji ambayo itasaidia kuzuia mafuriko kwa wakazi walio maeneo ya mto kizinga ikiwemo ujenzi wa mfereji wa Kwashego ambao mpaka sasa umekamilika kwa asilimia 70%.
Akizungumza na waandishi wa habari, Mwenyekiti wa bodi ya ushauri TARURA, Injinia Frolian Kabaka amesema haya juu ya utekelezaji wa miradi hiyo.
Aidha bodi ilifika kukagua mradi wa kituo cha Afya cha buza, ambacho kimeshakamilika na kimeanza kutumika.
Miradi mingine inayohusisha manispaa ya Temeke ni pamoja na mradi wa ujenzi wa bonde la gerezani, maboresho ya miundombinu ya jamii kata ya kilakala na Keko, maboresho ya miundo mbinu ya jamii ya mtoni,ujenzi wa barabara za chang’ombe, mchicha , temeke na mbagala, maboresho ya miundo mbinu buza ambayo itaunganisha ukanda wa mbagala na ilala, lakini pia ununuzi wa magari 20 ya kubebea taka na makontena 65 ya kuhifadhia Taka.
Bodi imepanga kumalizia ziara zake kesho tarehe 8 ya mwezi oktoba kwa kukagua miradi ya manispaa ya Kinondoni na Ilala.

Пікірлер: 8
@edwinfernandes8881
@edwinfernandes8881 4 жыл бұрын
Hapo sawa kabisa ...mfefanya ukaguzi kwa weledi na sio viongozi wa dini
@MdEmon-yn4cw
@MdEmon-yn4cw 4 жыл бұрын
mashaa Allah Tanzania yangu yazidi kupendeza
@mukambi3278
@mukambi3278 4 жыл бұрын
Kazi nzuri Mwananchi digital, kuna maelezo ya kutosha kimaandishi na ndani ya video. Media zingine wanaeka habari vipande yani mtu unabaki na maswali mengi kuliko majibu. Wanaeka alichoongea kiongozi tu wala hujui aliulizwa nn na wala anaeleza nn.
@mavuzijiwe6805
@mavuzijiwe6805 4 жыл бұрын
Safi sana serikali ya Awamu ya 5
@abushaddad989
@abushaddad989 4 жыл бұрын
Safii
@mimimoop2617
@mimimoop2617 4 жыл бұрын
Tanzania mpya
@smukelomkhize9775
@smukelomkhize9775 3 жыл бұрын
Safi sana
@issayasosolo5463
@issayasosolo5463 4 жыл бұрын
Kagueni yote halafu tupikie pilau sawa
HOTELI YA NYOTA TANO YAFUNGULIWA JIJINI DAR ES SALAAM,
5:16
Uwekezaji TV
Рет қаралды 13 М.
Новый уровень твоей сосиски
00:33
Кушать Хочу
Рет қаралды 4,2 МЛН
ASKARI WA FFU WAZINGIRA JIJI LA DAR, YADAIWA MAANDAMANO CHANZO
3:56
Mwananchi Digital
Рет қаралды 17 М.
If You Know These 15 Words, Your English is EXCELLENT!
7:39
Brian Wiles
Рет қаралды 2,3 МЛН
Private Equity’s Ruthless Takeover Of The Last Affordable Housing In America
13:23
CHADEMA YATANGAZA NJIA ZITAKAZOTUMIKA KWENYE MAANDAMANO
2:10
Mwananchi Digital
Рет қаралды 3,3 М.
NIATARI KATIKA JIJI LA BARAKA FIZI DRC.
15:01
Mmunga ML TV
Рет қаралды 27 М.
BlackRock: The Conspiracies You Don’t Know
15:13
More Perfect Union
Рет қаралды 395 М.
Mpango wa Kuendeleza Jiji la Dar es salaam miundombinu Ilala, Temeke na Kinondoni(BRT mpya )
13:58
Advanced Engineering Solutions Ltd Tanzania
Рет қаралды 41 М.