Рет қаралды 12,336
Imekuwa ni ziara yenye gumzo baada ya Rais wa Urusi, Vladmir Putin kuzuru China kwa siku mbili na kuteta na mwenyeji wake Rais Xi Jinping mjini Beijing.
Ajenda kubwa ambayo wameiweka hadharani baada ya kukutana kwao ni suala la vita vinavyoendelea nchini Ukraine kwa zaidi ya miaka miwili sasa huku wakisema mgogoro huo unahitaji suluhisho la kisiasa.
Lakini inafahamika kuwa wamekuwa na mazungumzo juu ya uhusiano wao wanaosema unazidi kuimarika na watauendeleza.
Katika uchambuzi huu tutaangalia ajenda za mataifa haya mawili na je zina maana gani kwao, kwa mahasimu ama washindani wao wa mataifa ya Magharibi na Dunia kwa ujumla wake?