Рет қаралды 76,943
Hoja ya Mbunge wa Viti Maalum, Halima Mdee aliyetaka Bunge lijadili utekelezaji wa miradi ya ujenzi wa barabara kwa EPC+F imechangamsha mjadala wakati Bunge likiwa limeketi kama kamati kujadili mafungu ya bajeti ya Wizara ya Ujenzi kwa mwaka wa fedha 2024/25.
Mjadala huo umejiri leo Mei 30, 2024 jioni huku Spika wa Bunge Dk Tulia Ackson akimbananisha Waziri wa Fedha, Dk Mwigulu Nchemba afafanue utekelezaji wa EPC+F huku Mbunge wa Kisesa, Luhaga Mpina akichuana vikali na Waziri wa Uchukkuzi ambaye aliwahi kuwa Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Profesa Makame Mnyaa Mbarawa wakishukiana kwenye mjadala huo.